Arakinida
Buibui ni oda ndani ya arakinida
Buibui ni oda ndani ya arakinida
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropodi (Wanyama bila uti wa mgongo wenye mwili wa vipingili na miguu yenye viungo)
Nusufaila: Chelicerata (Arthropodi wenye mwili wa mapande mawili na maungo mawili mbele ya domo)
Ngeli: Arakinida (Arthropodi wenye miguu minane)
Ngazi za chini

Nusungeli na oda
Nusungeli:

Oda:

Arakinida ni ngeli ya wanyama wasio na utimgongo. Kiasi wanafana na wadudu lakini wana miguu nane badala ya sita. Katika uainishaji wa kisayansi wamepangwa kama oda kati ya arithropoda.

Aina kati yao zinazojulikana zaidi ni buibui pamoja na nge na visusuli. Wadogo kati yao ni kupa na funduku.

Miili huwa na mapande mawili ambayo ni kichwa pamoja na kidari mbele na tumbo nyuma. Ila tu kwa funduku pande zote mbili hazionekani vizuri maadamu zimekua kama sehmu moja. Tabia inayoonekana vizuri ni miguu nane. Hata hapa funza za funduku wengi wana miguu sita tu.

Aina nyingi huwa na miiba ya sumu inayoweza kuuma. Kazi yake ni kusaidia uvindaji wa wanyama wengine lakini kwa spishi kadhaa sumu ni hatari hata kwa viumbe vikubwa kama binadamu akidungwa.


Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Arakinida kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.