Baekje au Paekche (Tamka pɛk̚tɕe) (18 KK – 660 KE) ulikuwa ufalme uliopo mjini kusini-magharibi mwa nchi ya Korea. Hii ilikuwa moja kati ya Falme Tatu za Korea, pamoja na Goguryeo na Silla.

Historia ya Korea.
Ufalme wa Korea
Baekje
  1. Onjo 18 BCE–29 CE
  2. Daru 29–77
  3. Giru 77–128
  4. Gaeru 128–166
  5. Chogo 166–214
  6. Gusu 214–234
  7. Saban 234
  8. Goi 234–286
  9. Chaekgye 286–298
  10. Bunseo 298–304
  11. Biryu 304–344
  12. Gye 344–346
  13. Geunchogo 346–375
  14. Geungusu 375–384
  15. Chimnyu 384–385
  16. Jinsa 385–392
  17. Asin 392–405
  18. Jeonji 405–420
  19. Guisin 420–427
  20. Biyu 427–455
  21. Gaero 455–475
  22. Munju 475–477
  23. Samgeun 477–479
  24. Dongseong 479–501
  25. Muryeong 501–523
  26. Seong 523–554
  27. Wideok 554–598
  28. Hye 598–599
  29. Beop 599–600
  30. Mu 600–641
  31. Uija 641–660

Baekje ilianzishwa na Onjo, mtoto wa tatu wa mwanzilishi wa Goguryeo Jumong na So Seo-no, mjini Wirye-sung (Seoul ya leo). Baekje, kama jinsi ilivyo Goguryeo, alidai kuuchukua Buyeo, nchi ilioanzishwa katika Manchuria ya leo kunako kipindi cha kuanguka kwa Gojoseon.

Baekje imepata mapigano tofauti na kuamua kuungana na Goguryeo na Silla wakiwa kama falme tatu zilizoweza kueneza kudhitibi peninsula. Kwenye kilele chake cha karne ya nne, Baekje imeweza kudhitibi baadhi ya kolono huko Uchina na sehemu kubwa ya magharibi mwa Peninsula ya Korea, na vilevile Pyongyang. Ikaja kuwa na nguvu sana kwa upande wa kanda ya bahari, kwa uhusiano wa kisiasa na kibiasha na Uchina na Japani.

Mnamo mwaka wa 660, ikajakuangushwa na nguvu ya muungano baina ya Silla na Nasaba ya Tang ya Uchina, ikajisalimisha kwa Muungano wa Silla.

Historia hariri

Uenezi hariri

 
Korea in 375, Upanuzi mkubwa wa nchi ya Baekje.

Wakati wa utawala wa Mfalme Goi (234–286), Baekje ikawa imejiendeleza kabisa ufalme wake, kama jinsi ilivyoendelea kuleta makubaliano mazuri ya Mahan. Mnamo 249, kulingana na maandishi ya kale ya Kijapani ya Nihonshoki, uenezi wa Baekje ulifika hadi mashariki mwa Gaya, maeneo ya bonde la Mto Nakdong. Baekje ilielezewa kwa mara ya kwanza kama ufalme kwenye rekodi za Kichina mnamo 345. Mpango wa kwanza wa kiplomasia kutoka Baekje ulifikia hadi huko nchini Japani kunako 367 (kwa mujibu wa Nihon Shoki : 247).

Mfalme Geunchogo (346–375) alipanua maeneo ya Baekje kwa upande wa kaskazini kwa kupitia vita dhidi ya Goguryeo, wakati anaanza kuchukua mamlaka ya jamii za Mahan zilizobakia huko mjini kusini. Wakati wa utawala wa Geunchogo, maeneo ya Baekje yalikuwemo upande zaidi ya magharibi mwa Peninsula ya Korea (kasoro mikoa miwili tu ya Pyeongan), na mnamo 371, Baekje ikashindwa na Goguryeo huko Pyongyang. Baekje ikaendelea kufanya shughuli za kiabiashara na Goguryeo, na kupelekea kuchukua tamaduni za Kichina na teknolojia. Ubudha ukawa dini rasmi ya kwanza nchini mnamo 384.

Baekje ikawa ina nguvu kwa upande bahari na kuendeleza mahusiano mazuri ya kihisani na viongozi wa Kijapani wakati wa Kipindi cha Kofun, ikabadilisha athira za kitamaduni kibara huko Japani. Mfumo wa uandikaji wa Kichina, Ubudha, uliendelea siku hadi siku, sherehe za mazishi, na mambo mengine ya kitamaduni yalianzishwa na wakubwa, mafundi, wasomi, na mamonki kwa kupitia mahusiano yao mazuri.[1]

Wakati wa kipindi hicho, beseni la Mto Han limebaki kama ardhi-moyo wa nchi.

Tanbihi na marejeo chini ya kurasa hariri

  1. "Korean Buddhism Basis of Japanese Buddhism," Seoul Times, 18 Juni 2006; "Buddhist Art of Korea & Japan," Asia Society Museum; "Kanji," JapanGuide.com; "Pottery Archived 29 Oktoba 2009 at the Wayback Machine.," MSN Encarta; "History of Japan," JapanVisitor.com.

Tazama pia hariri

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: