Cangrelor

kiwanja cha kemikali

Cangrelor, inayouzwa kwa jina la chapa Kengreal miongoni mwa mengine, ni dawa inayotumiwa kwa wale wanaopitia tiba ya kupenya mishipa ya moyo iliyoziba kupitia ngozi (percutaneous coronary intervention) ili kuzuia kuganda kwa damu.[1] Dawa hii inatumika pamoja na aspirini[1] na inatolewa kwa njia ya sindano kwenye mshipa.[2]

Madhara yake ya kawaida ni pamoja na kutokwa na damu na upungufu wa kupumua.[1] Madhara yake mengine yanaweza kujumuisha athari za mzio.[1] Usalama wa matumizi yake katika ujauzito hauko wazi.[2] Dawa hii ni kizuizi cha P2Y <sub id="mwHw">12</sub> ambacho huzuia chembe za damu za pletleti kushikamana pamoja.[2][1]

Canrelor iliidhinishwa kwa ajili ya matumizi ya kimatibabu nchini Marekani na Ulaya mwaka wa 2015.[2][1] Nchini Uingereza, miligramu 50 hugharimu Huduma ya Afya ya Kitaifa (NHS) takriban £250 kufikia mwaka wa 2021.[3] Kiasi hiki nchini Marekani kinagharimu takriban dola 830 za Marekani.[4]

Marejeo

hariri
  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 1.4 1.5 "Kengrexal". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 17 Aprili 2021. Iliwekwa mnamo 29 Desemba 2021.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. 2.0 2.1 2.2 2.3 "Cangrelor Monograph for Professionals". Drugs.com (kwa Kiingereza). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 21 Januari 2021. Iliwekwa mnamo 29 Desemba 2021.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. BNF 81: March-September 2021. BMJ Group and the Pharmaceutical Press. 2021. uk. 225. ISBN 978-0857114105.
  4. "Kengreal Prices, Coupons & Patient Assistance Programs". Drugs.com (kwa Kiingereza). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 17 Aprili 2021. Iliwekwa mnamo 29 Desemba 2021.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Cangrelor kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.