Dadu ni kidude ambacho kwa kawaida kina umbo la mchemraba lakini kuna aina nyingine pia. Inatumiwa kwa kuirusha katika michezo ya bahati au pia katika mchezo ambako namba inahitajika kwa njia ya kubahatika.

Dadu ya pande sita
Dadu zenye maumbo mbalimbali

Dadu ya kawaida huwa na pande sita na namba kwenye ya kila upande. Kwa kawaida namaba hizi ni 1, 2, 3, 4, 5 na 6. Jumla ya namba za pande mbili za kinyume huwa ni 7.

Dadu inarushwa kwenye sehemu tambarare ama mezani au kwenye sakafu ya chumba. Namba au alama inayofika juu ni ya kubahatika. Kurushwa kwa dadu kunatokea ama kwa mkono au baada ya kutikisisha ndani ya chombo.

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: