David Mathayo David

David Mathayo David (amezaliwa 24 Julai, 1969) ni Mbunge katika Bunge la Tanzania.

Chanzo hariri

Jina
Jina la kwanza ni Mathayo David Msuya. Ila baada ya kuingia anga za siasa, aliamua kulibadili jina lake kuwa Mathayo David Mathayo na kuondoa jina la ukoo "Msuya" ambalo ni jina la baba yake halisi David Msuye aliyewahi kuwa waziri mkuu.

Masomo
Matayo David Msuya alisoma Tosamaganga Iringa, alifanya CBG (1989-91) aliishi bweni la Mwenge. Uwezo wake wa kimasomo haukuwa mkubwa ila alishangaza wenzanke na waalimu alipopata daraja la kwanza kwa pointi 7. Alipata msaada sana kutoka kwa kaka yake aliyekuwa akifundisha chuo cha ualimu Mkwawa, Iringa.
Matayo ulikwenda JKT itende, Mbeya. Baada ya hapo, alichanguliwa kwenda kusoma Makerere Uganda kwa kupitia mfuko wa mwalimu Nyerere. Mathayo alinufaika kwa fedha hizo ila hakwenda Uganda, akaamua kusoma SUA ya tiba ya mifugo (Bachelor of Veterinary Medicine) mwaka 1993-1997. Huko SUA Matayo alikuwa ni mwanafunzi pekee aliyekuwa na radio yenye double deck, (system) na TV set. Uwezo wa kifedha ulisaidia kumpa Mathayo maisha ya kifahari chuoni SUA ambapo alikuwa na wasichana kadhaa ikiwa ni pamoja na Mugros na Betty Manase

Mwanzo wa siasa
Siasa alizianza rasmi mwaka 1995 alitumia TV yake kwenda kuonyesha vijijini madhara ya vyama vingi, alitumia mapigano ya Rwanda na Burundi kama kutishia wananchi wasikubali upinzani na kipindi kile wananchi walikuwa wepesi kuelewa kumbuka TV hazikuwa nyingi Tanzania kipindi kile. Alijijengea umaarufu sana ndani ya chama mkoani Morogoro na kitaifa. Aligombea ujumbe wa NEC mkoa wa Morogoro kundi la vijana alishinda. Mathayo alimaliza SUA 1997 na kupata kazi ya kufundisha chuo kimoja huko Serowe Botswana. Kwa kuwa mjumbe wa NEC alikuwa karibu na akina Lowasa, JK na vingunge wengine aliweza kuwa anaonana na akina Makamba na akawa ni mwanamtandao. Wakati huo Matayo alikuwa akirudi Tanzania kufanya shughuli zake za kisiasa wakati bado ni mwajiriwa wa serikali ya Botswana. Kwa mfano wakati mmoja alirudi Tanzania na kuwahamasisha wanafunzi wa SUA (kama 200 hivi) na kuwapeleka Dodoma kupokea kadi za CCM chini ya mwenyekiti wa CCM Mkapa. Wanafunzi walahidiwa wangepatiwa ajira kwa kufanya hivyo. Hii ilimjenga sana Matayo ambaye aliisha kuwa maarufu kwenye ofisi za chama Dodoma, kama mjumbe wa NEC na mkutano mkuu. Mwaka 2000 aligombea Ubunge Same Magharibi na kushinda na kuteuliwa kuwa waziri mdogo. Wakti huu aliisha tamka kwamba amesomea Afrika Kusini digrii ya falsafa (PhD). Prof Msolla wakati aliyekuwa waziri wa elimu ya juu na sayansi ambaye aliwahi kufundisha SUA alimjua sana Matayo na alimwita Matayo na kumuuliza kuwa PhD alifanya lini na wapi na pia aletee PhD thesis yake. Prof Msolla alisema "Matayo aliogopa sana na alikili mbele yangu, kuwa Prof mimi nimetumia hii title kisiasa zaidi, sina MSc wala PhD”1.

Kashfa ya vyeti bandia
Dr Mathayo ni mmoja wa wabunge vijana waliochaguliwa na Raisi Kikwete kuwakilisha ngwe yake ya "Nguvu mpya" kama naibu waziri. Katika awamu hii Kikwete alionekana amechagua vijana wenye vipaji na elimu. Vyeti vya Mathayo's zimeleta kizaazaa tangu alipochaguliwa kwenye uwaziri mwaka 2005. Matayo alihitimu chuo kikuu cha Kilimo (SUA) mwaka 1997 kama daktari wa mifugo. Baada ya hapo alitoka nje ya nchi kwenda kutafuta ajira Botswana ambako aliajiriwa na serikali ya Botswana kama mwalimu kweny chuo cha kilimo huko Serowe. Mathayo anadai kwa mwaka huo huo alianza digrii ya MSc 1998-2001, halafu PgDip (2000-2001), na PhD (2001-2003). Watu wengi wanaomfahamu ikiwa ni pamoja na waalimu wake wa SUA wanashangaa Mathayo aliwezaje kusomea vyeti vyote hivyo kwa muda wa miaka mitano huku akifanya kazi kama mtumishi wa serikali Botswana? Pia kashfa kwamba alikuwa akipokea mishahara miwili ya uwaziri na utumishi wa serikali ya Botswana haijajibiwa hadi leo.

1. http://www.parliament.go.tz/bunge/mpcv.php?vpkey=376 Archived 16 Julai 2011 at the Wayback Machine. 2. http://www.jambonetwork.com