Destiny ni jina la kutaja wimbo ulioimbwa na kutungwa na msanii wa muziki wa hip hop kutoka nchini Tanzania - M-Rap. Wimbo huu amemshirikisha msanii wa Ragga Riddim/Bongo Flava Deddy. Maudhui ya kibwagizo cha wimbo huu ni ya Ragga, umeufanya kuwa wimbo pekee nchini Tanzania kuwa na kiitikio kizuri cha ragga kuliko zote zilizowahi kutolewa. Wimbo umetayarishwa na Pancho Latino akiwa na Hermy B.. Wimbo ulitolewa wiki tatu tu baada ya msanii huyu kuingia mkataba na B-Hits Music Group kunako mwezi wa Januari 2013.

“Destiny”
“Destiny” cover
Single ya M-Rap akimshirikisha Deddy
kutoka katika albamu ya Destiny
Imetolewa 2013
Muundo CD
Imerekodiwa 2012/2013
Aina Hip hop
Urefu 4:06
Studio B-Hits Music Group
Mtunzi M-Rap
Mtayarishaji Pancho Latino na Hermy B.
Mwenendo wa single za M-Rap akimshirikisha Deddy
Destiny
(2013)
Attention
(2013)

Deddy, amefanya Ragga ya Tanzania kuwa katika ramani. Mashairi yanataja au yanasisitiza usikate tamaa katika maisha. Hujui nini Mungu kakupangia, kama una nia na jambo fulani, basi amini utafanikiwa.

Historia hariri

Mashairi hariri

Mashairi yanataja au yanasisitiza usikate tamaa katika maisha. Hujui nini Mungu kakupangia, kama una nia na jambo fulani, basi amini utafanikiwa. Kutokana na uchungu alionao moyoni mwake katika kuhakikisha maisha yanaenda vyema, M-Rap alisema hivi:

DESTINY ni wimbo ambao unaelezea kila kitu ambacho kimetokea katika maisha yangu ya muziki - kwani nilipata vikwazo sana. Awali nilikuwa chini ya A.M RECORDS kwa MANEKE kwa takribani miaka mitatu, si haba niliyoyapata ninashkuru sana... Nikakosa sapoti kutoka kwa baba akisema kwamba muziki ni uhuni. Mama yangu mzazi amenisapoti ingawa sio kifedha kutokana na hali halisi ya uchumi wetu... Sala zake ninaamini ndio zimenifanya nisainiwe na studio kubwa B 'HITS chini ya PANCHO LATINO NA HERMY B...

Ile hatua ya kupata mkataba ni hatua kubwa moja niliopiga ndio ikanifanya niandike DESTINY Kwani nilipenda watu wajue nimepitia yapi mpaka nilipo... Kila kitu nilichoimba mle ni kweli sababu nikikumbuka pia nilishawahi kupuuzwa katika studio tofauti za hapa DAR ,SEMA niliapa na nikasema ndoto yangu lazima iwe kweli...nakumbuka nilikuwa nazunguka kwenye hayo mastudio nikiwa na ndala zilizonifanya nionekane mchafu na kutokuwa na mwonekano wa kisanii labda ndio kilichofanya nipuuzwe...

M-Rap
Mpangilio wa mashairi

DESTINY:Beti ya 1:

Intro:Jah ndo anapanga DESTINY If you have a dream know that you can make it#Trust me,M-RAP am on it... remember black africans. movement they made it Usiseme najaribu ondoa usemi ule wa maybe*4,Martin Luther King made the Africans united Remember black African movement they made it Usiseme najaribu ondoa usemi ule maybe Martin Luther King made the africans united Mungu akishapanga binadamu ye ni nani?! Aah,sema sirudi tena Pamoja we una nguvu mtegemee Mungu sana Wenye money,power ni watoto kwa Maulana Uliyemkosa hujachelewa,haukujua unachofanya Baba alijua nimepotea Akawa na imani kwenye giza naelekea Akasema mziki uhuni,kumbe talanta mekalia Bila ya kujua ma mama ananiombea Thinking of the future,carin of da present Eti four siwezi vuka nitakuwa mpiga debe Muhuni,kibaka,mabaya acha waseme Uchungu alopata mama sijui vipi niseme


DESTINY: Beti ya 2:

Dear LORD says ,no work no food Without hustlin,there comes no good Nkaendelea strugglin,sometimes no food Najitazama kwenye kioo,merudi home jasho full Aaah sikuwa na demu,nlikuwa lonely Sikuona mwanga ni giza kwa machoni Mziki mgumu nusu niache niwe msomi nikaamini itawaka in the mornin God bless me i met HERMY na LATINO Ndipo nikasign deal nikamwaga wino Girls na machizi like oouw!yu know TZ mpaka KENYA BHITZ we on 1 my dream real man came true Artist MAMA am proud of you Kama una lengo hustle utakuwa juu Weka jitihada usimsahau aliye juu.

Marejeo hariri

Viungo vya Nje hariri