Msokotaji-hariri

(Elekezwa kutoka Embioptera)
Msokotaji-hariri
Msokotaji-hariri asiyetambulishwa
Msokotaji-hariri asiyetambulishwa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wa pingili na miguu ya kuunga wasio na ugwe wa mgongo kama wadudu, nge, buibui)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
(bila tabaka): Dicondylia (Wadudu walio na mandibula zenye condyle mbili)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Linnaeus, 1758
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Lang, 1888
Oda: Embioptera
Lameere, 1900
Ngazi za chini

Familia 10:

Wasokotaji-hariri ni wadudu wadogo wa oda Embioptera (embios = -epesi, ptera = mabawa) ambao wana tezi kwenye miguu ya mbele zinazotumika kwa kusokota hariri. Hutumia hariri hii ili kuumba njia na vyumba juu ya miamba, juu ya gome la miti au ndani ya takataka za majani. Mwili wa wadudu hawa ni kinamo na una umbo wa mcheduara. Hii inarahisisha maisha yao ndani za njia za hariri. Madume ya spishi nyingi wana mabawa lakini madume ya spishi nyingine na majike wote hawanayo.

Wasokotaji-hariri huishi ndani ya njia za hariri takriban saa zote. Madume wanatoka njia hizi ili kutafuta majike, na majike wanatoka ili kutafuta chakula. Wakipata chakula majike wanaumba njia mpya za hariri juu ya chakula hiki. Hula takataka za majani, vigoga, gome na kuvumwani. Madume hawakuli.

Spishi kadhaa za Afrika ya Mashariki hariri

  • Chirembia baringoa
  • Chirembia leechi
  • Chirembia micropallida
  • Dihybocercus confusus

Picha hariri

  Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Msokotaji-hariri kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  Makala hiyo kuhusu "Msokotaji-hariri" inatumia jina ambalo halijakuwepo kwa lugha ya Kiswahili. Jina hili linapendekezwa kwa jina la mnyama huyu au wanyama hawa amba(ye)(o) ha(wa)na jina kwa sasa.

Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.
Kamusi za Kiswahili hazina jina kwa mnyama huyu au wanyama hawa.