Enekia Lunyamila

Mchezaji wa mpira wa miguu Tanzania

Enekia Kasonga Lunyamila, (alizaliwa tarehe 20 Aprili 2002) ni mchezaji wa mpira wa miguu wa nchini Tanzania, ambaye anacheza kama mshambuliaji katika klabu ya AUSFAZ, katika Ligi ya Wanawake ya Morocco, na Timu ya Taifa ya wanawake Tanzania.[1][2]

Enekia Kasonga Lunyamila
Maelezo binafsi
Tarehe ya kuzaliwa 20 Aprili 2002
Mahala pa kuzaliwa    Kigoma, Tanzania
Nafasi anayochezea Mshambuliaji
Timu ya taifa
Timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania

* Magoli alioshinda

Ushiriki Kimataifa hariri

Lunyamila aliichezea timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 20 mwaka 2019 na 2020. Aliwea kufunga mabao 4 na kuifanya timu kushinda mashindano ya Wanawake ya COSAFA chini ya miaka 20 ya 2019. Mwisho wa mashindano alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mashindano.

Kasonga aliichezea timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania wakati wa mashindano ya wanawake ya COSAFA 2020 na mashindano ya wanawake ya COSAFA 2021.[3][4][5] Alifunga bao pekee, bao la ushindi katika fainali ya 2021 dhidi ya Malawi na kuifanya Tanzania kushinda michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia yake.[6][7]

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Enekia Lunyamila kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.