Gabon

(Elekezwa kutoka Gaboni)


Gabon, kirasmi Jamhuri ya Gabon, ni nchi huru ya Afrika ya Magharibi ya kati.

Jamhuri ya Gabon
République Gabonaise (Kifaransa)
Kaulimbiu ya taifa:
Union, Travail, Justice (Kifaransa)
"Umoja, Kazi, Haki"
Wimbo wa taifa: La Concorde (Kifaransa)
"Mapatano"
Mahali pa Gabon
Mahali pa Gabon
Ramani ya Gabon
Ramani ya Gabon
Mji mkuu
na mkubwa nchini
Libreville
0°23′ N 9°27′ E
Lugha rasmiKifaransa
MakabilaKupita makabila 40
SerikaliJamhuri
yenye baraza la majeshi
 • Kaimu RaisBrice Oligui Nguema
Eneo
 • Eneo la jumlakm2 267 668
Idadi ya watu
 • Kadirio la 20232 397 368
Pato la taifaKadirio la 2023
 • JumlaPunguko USD bilioni 19.319
 • Kwa kila mtuPunguko USD 8 831
Pato halisi la taifaKadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 41.922
 • Kwa kila mtuOngezeko USD 19 165
Maendeleo (2021)Ongezeko 0.706 - juu
SarafuFaranga ya CFA
Majira ya saaUTC+1
(Afrika ya Magharibi)
Msimbo wa simu+241
Msimbo wa ISO 3166GA
Jina la kikoa.ga

Imepakana na Guinea ya Ikweta, Kamerun, Jamhuri ya Kongo na Ghuba ya Guinea.

Nchi hii ina umma mdogo, madini na mali kwa wingi, na wafanyabiashara kutoka nchi za kigeni wameweza kufanya Gabon iwe nchi yenye maendeleo makubwa.

Jiografia hariri

Maeneo ya utawala hariri

Gabon imegawiwa katika mikoa 9 nayo ina jumla ya wilaya (départements) 37.

Mikoa ni:

Historia hariri

 
Aliyekuwa Rais Omar Bongo Ondimba wa Gabon (kushoto) akiwa Washington, USA.

Jamhuri ya Gabon, tangu kupata uhuru kutoka Ufaransa tarehe 17 Agosti 1960, imeongozwa na Rais watatu, Léon M'ba, El Hadj Omar Bongo ambaye amekuwa kiongozi kutoka mwaka wa 1967 hadi kifo chake (2009: ndiye aliyekuwa kiongozi barani Afrika aliyeshikilia uongozi kwa muda mrefu zaidi), halafu mwanae Ali aliyepinduliwa na wanajeshi tarehe 30 Agosti 2023.

Siasa hariri

 
Nyumba ya baraza, Libreville

Mwaka wa 1990 Gabon ilianza demokrasia ya vyama vingi na katiba ya kidemokrasia ili ruhusu ukweli wa uchaguzi na uwajibikaji wa idara za serikali, lakini hali iliendelea kuwa karibu ileile.

Uchumi hariri

Gabon ni nchi yenye neema sana kuliko nchi jirani. Uchumi wake, hasa chumo cha umma, ni mara nne ya nchi za Afrika kusini kwa Sahara. Hii hasa ni kwa sababu ya uzalishaji wa mafuta ambao umeleta utajiri na mali, lakini usambazaji wa mali hii ya mafuta bado umedhoofika.

Gabon ilikuwa mwanachama wa Muungano wa Nchi Zinazouza Mafuta (OPEC) kutoka mwaka wa 1975 mbaka 1995.

Mwaka 1990, udhaifu wa pesa CFA frank uliacha Gabon katika shida ya kulipa deni za kimataifa; Ufaransa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) wameipa Gabon mkopo na usaidizi kwa uelewano kwamba Gabon itageuza uchumi wake barabara.

Watu hariri

Yasemekana mambo ya mazingira yalifanya umma wa Gabon kutopanda kwa sensa kati ya miaka 1900 na 1940.

Ni nchi ambayo ina umma mdogo zaidi katika Afrika bara, na upungufu wa wafanyakazi ni mojawapo ya mambo yanayofanya hasa uchumi kutovuma zaidi.

Umma hasa kwa ujumla ni kama watu milioni 2.4.

Gabon hasa ina makabila zaidi ya 40 ambayo yana utamaduni na lugha tofauti lakini karibu wote (95%) ni wa jamii ya Bantu. Wafang ndio kabila kubwa zaidi nchini Gabon, wengine ni Wamyene, Wabandjabi, Waeshira, Wabapounou na Waokande.

Lugha ya Kifaransa ndiyo lugha rasmi ya taifa ambayo hutumika kwa mawasiliano (wakazi wanaoimudu ni 80%). Wafaransa 10,000 wanaishi Gabon, na Ufaransa unaathiri mambo ya kigeni, utamaduni na biashara nchini Gabon.

Upande wa dini, imekadiriwa kwamba 75.6% za wakazi ni Wakristo (hasa Wakatoliki), 12.2% ni Waislamu (hasa wageni), na 5.7% wanafuata dini asilia za Kiafrika (Bwiti).

Utamaduni hariri

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

  • David E. Gardinier and Douglas A. Yates, Historia elekezo ya Gabon, tolezi ya 3. (The Scarecrow Press, Inc., 2006)
  • David E. Gardinier, Kamusi ya Historia ya Gabon, tolezi ya 2. (The Scarecrow Press, Inc., 1994) – kazi inayohusu maelezo biografia ya vifaa 1,453
  • James F. Barnes, Gabon: Beyond the Colonial Legacy (Boulder: Westview, 1992)

Viungo vya nje hariri

Serikali hariri

Habari hariri

Uchambuzi hariri

Koo na makabila hariri

Maelekezo hariri

Utalii hariri


Nchi za Afrika  
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Gabon kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.