Galus I wa Clermont

Galus I wa Clermont (Clermont-Ferrand, leo nchini Ufaransa, 489 hivi - Clermont-Ferrand, 553 hivi) alikuwa askofu wa 16 wa mji huo kuanzia mwaka 527 hadi kifo chake[1].

Mtoto wa makabaila, alikataa ndoa akawa mmonaki mnyenyekevu na mpole. Kwanza alifanywa padri, halafu askofu, akaongoza kwa ufanisi mkubwa[2], kama ilivyoandikwa na Gregori wa Tours, aliyekuwa mwanafunzi wake na mwana wa ndugu yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 14 Mei[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/53140
  2. Jones, Terry. Gall. Patron Saints Index. Jalada kutoka ya awali juu ya 2007-11-09. Iliwekwa mnamo 2007-11-09.
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.