Hussein ibn Ali[1] (kwa Kiarabu: حسين بن علي‎; 11 au 13 Januari 626 BK10 Oktoba 680 BK, sawa na 3 Shaabani 4 BH - 10 Muharram 61 BH; 3 شعبان 4 هـ - 10 محرم 61 هـ) alikuwa mjukuu wa Mtume Muhammad akitazamwa kama imamu wa kwanza wa Washia. Alizaliwa mjini Makka, baba yake alikuwa Ali ibn Abi Talib (khalifa wa nne na mama yake Fatimah Zahra binti Muhammad. Kaka yake alikuwa Hasan ibn Ali imamu wa pili wa Washia.

Msikiti wa Kaburi la Imamu Hussein mjini Karbala.
Taswira ya Kiajemi inayomwonyesha Hussein katika mapigano ya Karbala.

Aliuawa katika Mapigano ya Karbala pamoja na wengi wa familia yake kwenye siku ya Ashura. Hivyo anatazamwa kama mfiadini, hasa kati ya Washia, na kukumbukwa kwenye sherehe za mwezi Muharram, hasa siku za Tasua na Ashura.[2]

Hussein ibn Ali ni muhimu sana kati ya Washia wanaomwangalia kama mtu mtakatifu kutokana na uhusiano wake wa karibu na mtume Muhammad na kama kielelezo kwa ushujaa katika mapigano ya Karbala. Washia wanamkumbuka na kukumsifu kwa upinzani wake dhidi ya Yazid I aliyekuwa khalifa wa Wamuawiya.

Marejeo hariri

  1. Jina lake linaandikwa pia Husayn, Husain, Hussain au Hossein kwa herufi za Kilatini
  2. Nakash, Yitzhak (1 January 1993). "An Attempt To Trace the Origin of the Rituals of Āshurā¸". Die Welt des Islams. 33 (2): 161–181. doi:10.1163/157006093X00063.
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Hussein ibn Ali kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.