Coordinates: 57°N 160°E / 57°N 160°E / 57; 160

Rasi ya Kamchatka (rus. полуо́стров Камча́тка poluostrov Kamchatka) ni rasi kwenye upande wa wa mashariki ya Urusi. Ina urefu wa kilomita 1,250 na eneo la 270,000 km².[1]

Rasi ya Kamchatka kwenye mashariki ya Urusi
Picha mbili za Kamchatka kutoka angani; kushoto: rasi wakati wa Juni, kuna mawingu mengi upande wa mashariki; kulia: rasi yote pamoja na bahari ya karibu imefunikwa kwa theluji na barafu wakati wa Januari.

Imeenea katika Bahari Pasifiki ikitenganisha Bahari ya Okhotsk na Pasifiki kubwa.[2]

Volkeno za Kamchatka zimeandikishwa katika orodha ya UNESCO ya urithi wa dunia.

Kiutawala ni sehemu ya mkoa wa Kamchatka Krai mwenye wakazi 322,079. Zaidi ya nusu ya wakazi hawa wanaishi katika miji miwili ya Petropavlovsk-Kamchatsky (waakzi 179,526) na Yelizovo (38,980).

Marejeo hariri

  1. Быкасов В. Е. Ошибка в географии // Известия Всесоюзного Географического Общества. — 1991. — № 6. (Kirusi)
  2. Kamchatka Peninsula. Encyclopædia Britannica. Iliwekwa mnamo 2008-02-20.
  • Gleadhill, Diana (2007), Kamchatka: A Journal & Guide to Russia's Land of Ice and Fire, Hong Kong: Odyssey Books, ISBN 978-962-217-780-2 .

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: