Kikosi Cha Mizinga

Kikosi Cha Mizinga ni kundi la Rap na HipHop ya Bongo linalotokea wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Kikosi Cha Mizinga
Nembo ya Kikosi Cha Mizinga.
Nembo ya Kikosi Cha Mizinga.
Maelezo ya awali
Asili yake Kinondoni,Dar es Salaam
Tanzania
Aina ya muziki Hip hip
Rap za kigumu
Hip hop za kisiasa
Miaka ya kazi 1998 -
Studio 41 Records
Ame/Wameshirikiana na Imam Abbas
Rado
Jay Moe
Wanachama wa sasa
Kara Pina
Gwalu Fukuda
Suma Lago
Msema Kweli
Bekham
Chatu Rage
Mau

Ni kundi linaloundwa na wasanii mahiri katika fani hii ya muziki wa Hip Hop nchini Tanzania. Kinara wa kundi hilo ni rapa Karama MASOUD almaarufu Mulla, Kubwa Lao, ama Kiboko ya Mabitozi. Zaidi ya muziki wa Hip Hop, kundi hilo lina familia na ukwasi mkubwa wa wasanii wa fani mbalimbali. Baadhi ya wanamuziki wa kundi hilo ni Gwalu Fukuda, Suma Lago, Bekham, MsemaKweli, Bekham, Chatu Rage, na mwanadada Mau.

Kundi hilo, kama ilivyo dhima ya hip hop ambayo ni kueleza ukweli na kuchangia kwenye maendeleo ya jamii, limejihusisha na bado linajihusisha na kupambana na matatizo anwai yanayoikabili nchi ya Tanzania kama vile ufisadi, tatizo la madawa ya kulevya, na uvunjifu wa haki za binadamu. Kwa hivi sasa kundi hilo linaendesha kampeni dhidi ya utumiaji wa madawa ya kulevya kwenye sanaa na nje ya sanaa ya muziki kwa ujumla.

Viungo vya nje hariri


  Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kikosi Cha Mizinga kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.