Kipini ni kijiji cha wavuvi kwenye pwani ya Kenya katika Kaunti ya Tana River. Iko kilomita 20 kusini mwa Witu kwenye mdomo wa Mto Tana unapoishia katika Bahari Hindi.

Ramani ya Kipini kwenye mdomo wa Mto Tana.
Mwambao wa Kipini.

Historia hariri

Kipini imetambuliwa kuwa mji wa kihistoria ya Waswahili katika Kenya ya leo. [1] Kuna mabaki ya makaburi yaliyojengwa kwa mawe ambayo yanafikiriwa kuwa na asili katika karne ya 11[2].

Katika karne ya 19 Kipini ilitajwa katika mkataba baina ya Ujerumani na Uingereza kama mpaka wa kaskazini wa maeneo ya Sultani wa Zanzibar yaliyotambuliwa nao, mbali na Lamu na miji kadhaa.[3] Hivyo ilikuwa pia kwa muda mpaka wa kaskazini wa koloni la Kenya kwenye pwani[4].

Baadaye wakati wa ukoloni Kipini ilikuwa makao makuu ya wilaya ya Lower Tana.

Marejeo hariri

  1. James de Vere Allen. “Swahili Culture and the Nature of East Coast Settlement.” The International Journal of African Historical Studies, vol. 14, no. 2, Boston University African Studies Center, 1981, pp. 306–34, https://doi.org/10.2307/218047.
  2. Coastal Culture Archived 20 Mei 2022 at the Wayback Machine., tovuti ya Kipini Conservancy, iliangaliwa Aprili 2022
  3. H. Brode: British and German East Africa, London 1911, uk. 4
  4. [British East Africa or IBEA, A History of the Formation and Work of the Imperial British East Africa Company], Appendix 1; London Chapman & Hall 1895