Bartimayo ni mmojawapo kati ya wachache ambao tunafahamu majina yao kati ya waliofaidika na miujiza ya Yesu, ingawa inawezekana si jina lake mwenyewe, bali ubini kama lilivyotafsiriwa "mwana wa Timayo".[1]

Yesu akimponya kipofu Bartimeo, kadiri ya Johann Heinrich Stöver, 1861.

Kipofu huyo alimlilia sana Yesu akimuita "Mwana wa Daudi", bila kujali makemeo ya watu wengine waliomdharau kama mkosefu aliyeadhibiwa na Mungu.

Habari yake inasimuliwa na Injili Ndugu zote tatu mwishoni mwa safari ya Yesu Kristo kwenda Yerusalemu ili kufa msalabani na kufufuka (Mk 10:46-52; Math 20:29-34; Lk 18:35-43).[2][3][4]

Papa Benedikto XVI alifananisha Kanisa lote na Bartimayo, kipofu aliyejaliwa kuona.[5]

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Vincent Taylor. The Gospel according to St. Mark. 1966 St. Martin's Press Inc. p 448.
  2. Jesus the Teacher: A Socio-Rhetorical Interpretation of Mark by Vernon K. Robbins 2009, ISBN 978-0-8006-2595-5 41-43.
  3. Vernon K. Robbins, “The Healing of the Blind Bartimaeus (10:46-52) in the Marcan Theology,” Journal of Biblical Literature 92 (1973), 224-243 [1]
  4. Bruce Robison, "Sermon, Sunday, October 25, 2009, Twenty-First after Pentecost, 2009, on Mark 10: 46-52 (RCL Proper 25B)," found at The Rector's Page. Accessed October 28, 2009.
  5. "Pontiff Urges African Church to Have Courage," October 25, 2009, from ZENIT's Web page Archived 16 Machi 2012 at the Wayback Machine., found at catholic.net website. Accessed October 28, 2009.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bartimayo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.