Kokoko-mlasamaki

Ndege mbuai wa familia Strigidae
Kokoko-mlasamaki
Kokoko-mlasamaki madoa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Strigiformes (Ndege kama bundi)
Familia: Strigidae (Ndege walio na mnasaba na bundi)
Nusufamilia: Striginae (Ndege walio na mnasaba na bundi)
Jenasi: Ketupa Lesson, 1830

Scotopelia Bonaparte, 1850

Spishi: Angalia katiba

Kokoko-walasamaki ni ndege mbuai wa jenasi Ketupa na Scotopelia katika familia Strigidae. Siku hizi wataalamu wengi wanawaainisha katika jenasi Bubo. Ndege hawa ni wakubwa kuliko bundi na wana mnasaba na kungwi.

Ndege hawa wana mgongo kwa rangi ya kahawa au kijivu pamoja na madoa meupe, na mbele yao ni nyeupe pamoja na madoa au michirizi nyeusi au kahawia. Spishi za Ketupa zina vishungi viwili vya manyoya vinavyofanana na masikio.

Kokoko-walasamaki wanatokea karibu na mito na maziwa katika misitu minene. Huwinda usiku na hula samaki hasa lakini amfibia na wanyama wadogo pia.

Jike huyataga mayai 1 au 2 lakini mara nyingi kinda moja aishi tu. Kwa kawaida tago lao ni kwenye mti mkubwa lakini katika shimo la mwamba pia.

Spishi za Afrika hariri

Spishi za mabara mengine hariri

Picha hariri