Mwangaza unaoonekana : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika ''''Uangavu''' ni tabia ya nyota inayosaidia kuzitofautisha. Kuna tofauti kati ya '''uangavu unaoonekana''' na '''uangavu halisi'''. Umbali kati ya vitu kw...' |
(Hakuna tofauti)
|
Pitio la 10:13, 10 Julai 2017
Uangavu ni tabia ya nyota inayosaidia kuzitofautisha. Kuna tofauti kati ya uangavu unaoonekana na uangavu halisi.
Umbali kati ya vitu kwenye anga la nje ni kubwa sana. Nyota kubwa kama iko mbali inaonekana hafifu, nyota ndogo kama iko karibu inaonekana angavu sana.
- Uang‘avu unaoonekana ni kipimo cha ukali wa nuru wa gimba la angani jinsi unavyoonekana kwa mtazamaji kwenye dunia yetu. Unatajwa kwa namba na kizio chake ni magnitudo, kifupi mag. Kadri uang‘avu ni juu namba yake ni ndogo. [1] Kitu ang‘avu zaidi angani ni jua letu kenye uang‘avu unaonekana wa -−26,73 mag. Nyota ya Rijili Kantori ( en:Alpha Centauri) inaonekana ang‘avu kushinda nyota kubwa zaidi ya Jibuta la Jauza kwa sababu iko karibu zaidi na dunia.
Kipimo cha magnitudo
Kwa kutaja kiasi cha uangavu wanaastronomia hutumia kizio cha "magnitudo". Neno hili la Kilatini linamaanisha "ukubwa".
Mifano ya uangavu unaoonekana na halisi
Nyota | Uang‘avu unaoonekana (m) |
Uang‘avu halisi (M) |
Umbali |
---|---|---|---|
Jua | −26,73 mag | +4,84 mag | 4,851·10−6 pc |
Shira (en:Sirius) |
−1,46 mag | +1,43 mag | 2,64 pc |
Vega |
+0,03 mag | +0,58 mag | 7,75 pc |
Sumbula (en:Spica) |
+1,04 mag | −3,51 mag | 81,3 pc |
Rijili Kantori (en:Alpha Centauri) |
+0,12 mag | −6,78 mag | 240 pc |
Dhanabu (en:Deneb) |
+1,25 mag | −7,24 mag | 499 pc |