Lugha : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
|||
Mstari 21:
== Tabia za lugha ==
Lugha huwa na tabia zifuatazo:
* Lugha huzaliwa: ni kutokana na lugha nyingine moja au zaidi zilizotangulia kuwepo.
* Lugha hukua: lugha hukua (kuongezeka kwa maneno, kuongezeka kwa idadi ya wazungumzaji, kuwa na mawanda mapana, kusanifiwa) kadiri inavyoendelea kutumiwa na jamii.
* Lugha hutohoa: lugha ina tabia ya kuchukua au kukopa maneno kutoka lugha nyingine.
* Lugha hufundishika: mtu yeyote anaweza kujifunza walau kiasi lugha yoyote hata kwa njia ya ufundishaji.
* Lugha huathiriana: lugha yoyote inaweza kuathiriwa na lugha nyingine.
* Lugha lazima ijitosheleze: kila lugha inajitosheleza kulingana na mahitaji ya jamii inayotumia lugha yenyewe.
* Lugha zina [[ubora]]: lugha zote ni bora hakuna lugha bora kuliko nyingine zote.
* Lugha hurithiwa: jamii hurithi lugha kutoka kizazi hadi kizazi.
* Lugha hufa: inapozidi mno kubadilika mwisho si yenyewe tena, lakini pia inapoachwa isitumike tena kwa kuwa wahusika wanapendelea lugha nyingine.
== Sifa za lugha ==
* Lugha lazima iwe inahusu binadamu
|