Liturujia ya Antiokia : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 1:
[[Image:HolyqurbonoSehion.jpg|thumb|[[Liturujia ya Kimungu]] ikiadhimishwa katika [[monasteri]] ya [[Mwinjili Marko|Mt. Marko]].]]
'''Liturujia ya Antiokia''', inayoitwa pia '''Liturujia ya Siria''', ni [[jina]] la taratibu za [[ibada]] ya [[Wakristo]] ambayo ina [[asili]] yake katika [[mji]] wa [[Antiokia]] wa [[Siria]] (siku hizi umo katika mipaka ya [[Uturuki]]) ambao katika [[karne ya 1]] ulikuwa kituo kikuu cha [[umisionari]] wa [[Kanisa]], halafu ukawa na [[shule ya teolojia]] muhimu kama ile shindani ya [[Aleksandria]] ([[Misri]]).
Wanaotumia liturujia hiyo ni hasa [[Kanisa la Kiorthodoksi la Siria]] na [[madhehebu]] yenye uhusiano naye [[Historia|kihistoria]] (hasa matawi ya [[Kanisa la Kiorthodoksi la Kisiria la Malankara]] kutoka [[India]]), na yale yaliyotokana nalo, yakiwa pamoja na [[Kanisa Katoliki la Kisiria]] na [[Kanisa Katoliki la Kimalankara]]. Kwa kiasi kikubwa liturujia hiyo ni pia ya [[Kanisa la Wamaroni]].
==Historia==
[[File:SyriacChurch-Mosul.jpg|right|thumb|Adhimisho la [[Kiorthodoksi la Kisiria]] katika monasteri ya [[Mosul]], (leo nchini [[Iraq]]), mwanzoni mwa [[karne ya 20]].]]
Liturujia hiyo ilitokana hasa na [[Liturujia ya Ugiriki|ile ya Kigiriki]] iliyotumiwa kwanza na [[Patriarki]] wa mji huo, lakini, baada ya [[farakano]] la mwaka [[451]] lililofuata [[Mtaguso wa Kalsedonia]], [[Tafsiri|ilitafsiriwa]] katika [[lugha]] ya [[Kiaramu]], iliyokuwa ya kawaida zaidi katika maeneo yote ya kandokando.
Matini ya Kiaramu ya zamani zaidi
Kuanzia [[anafora]] ya awali, iliyotafsiriwa kutoka ile ya [[Kigiriki]] ya [[Liturujia ya Mt. Yakobo|Mt. Yakobo]], zilitungwa nyingine nyingi, si chini ya 39.
[[Wakatoliki]] ndio waliofanya [[utafiti]] bora zaidi juu ya liturujia hiyo, wakitoa [[vitabu]] rasmi ili kupunguza fujo iliyojitokeza pengine kati ya [[Waorthodoksi wa Mashariki]]. Kati ya anafora hizo zote, wanazitumia [[Saba (namba)|saba]] tu.
Pengine masomo ya [[Biblia]] yanafanyika kwa [[Kiarabu]], lugha ya kawaida ya waamini wengi huko [[Mashariki ya Kati]]. Lakini waamini wengi zaidi wanaishi [[India]] kusini.
==Tanbihi==
Mstari 32:
* [http://www.epilgrim.org/syrian_liturgy.htm Syrian Liturgy] description and photos
* [http://docorient.com/index_gb.html Documentary film about Syriac Christians]
{{mbegu-Ukristo}}
[[Category:Liturujia]]
[[Category:Waorthodoksi wa Mashariki]]
[[Category:Kanisa Katoliki]]
|