Binadamu : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Mstari 60:
 
Chaguo letu binadamu linafanyika siku kwa siku kwa kuchukua misimamo mizuri au mipotovu kuhusu [[dini]] na [[maadili]]. “Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima” ([[Yoh]] 5:39-40).
 
Binadamu ni [[umoja]] wa mambo mawili: roho iliyoumbwa na Mungu moja kwa moja, na [[mwili]] ulioumbwa naye kwa njia ya [[wazazi]]. [[Maumbile]] hayo yanatakiwa kukamilika kwa kupokea na kutimiza [[upendo]] wa Mungu aliyesema, “’Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi’. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba” ([[Mwa]] 1:26-27).
 
Hivyo, mwili wetu ni muhimu, kwa sababu umeumbwa na Mungu, umetwaliwa na [[Mungu Mwana|Mwanae]] ili atuokoe, umehuishwa na [[Roho Mtakatifu]] atakayeutukuza siku ya [[Ufufuko|ufufuo]] kwa mfano wa Yesu. “Mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake. Je, hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye?… Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu?” ([[1Kor]] 6:13-16,19).
 
[[Utoto]]ni anasukumwa tu na [[haja]] za [[umbile]] lake, ambazo ni muhimu kwake na anazilenga bila ya kuhitaji juhudi.