Mwezi : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
Mstari 56:
Hata kama [[Warusi]] na Wamarekani walifikisha [[bendera]] zao mwezini, hakuna anayedai [[mali]] huko. Katika [[mkataba kuhusu anga za nje]] nchi 192 za dunia zimepatana ya kwamba mwezi utaangaliwa sawa na maeneo ya kimataifa ya [[bahari]]. Walipatana pia ya kwamba itakuwa marufuku kupeleka [[silaha]] kali kama [[bomu la nyuklia|za nyuklia]] angani. [[Taifa|Mataifa]] mengi ya dunia yamejiunga na [[mkataba]] huo, isipokuwa nchi chache hasa za [[Afrika]] hazikutia sahihi kama vile [[Tanzania]].
Lakini kuna watu binafsi wanaodai mali ya mwezi. Tangu mwaka 1980 yupo Mwamerika mmoja aliyefaulu kuandikisha Mwezi kwa jina lake kwenye ofisi ya msajili wa viwanda [[Mji|mjini]] [[San Francisco]] akiendelea kuuza hati za kumiliki maeneo mwezini. Kuna pia familia moja pale Ujerumani iliyorithi hati ambako mfalme wa Prussia kwenye mwaka 1756 alitoa zawadi ya Mwezi kwa mzee wao. Taasisi ya Sheria ya Anga za Nje ''(International Institute of Space Law)'' ilitoa tamko kuwa madai haya hayana msingi wa kisheria <ref>[http://www.iislweb.org/docs/IISL_Outer_Space_Treaty_Statement.pdf Statement by the Board of Directors of the International Institute of Space Law (IISL) on Claims to Property Rights Regarding the Moon and Other Celestial Bodies], International Institute of Space Law. 2004</ref>.
== Vyanzo ==
|