Chuo cha Kikristo cha Aleksandria : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Addbot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating interwiki links, now provided by Wikidata on d:q622189
Ukurasa umeelekezwa kwenda Shule ya Aleksandria
Tag: New redirect
Mstari 1:
#REDIRECT[[shule ya Aleksandria]]
'''Chuo cha Kikristo cha [[Aleksandria]]''' (au '''Shule ya Elimu ya Kikristo ya Aleksandria''') kilikuwa taasisi ya elimu ya Kikristo wakati wa karne za kwanza BK na kati ya vyuo vya kwanza vilivyofundisha imani ya kikristo kwa namna ya kitaalamu.
 
Kilianzishwa mnamo mwaka 190 na mwanzoni kusudi lake lilikuwa kuwaelimisha wapagani waliotafuta habari za imani mpya ya kikristo kabla ya ubatizo. Chuo cha Aleksandria kikaendelea haraka kuwa kitovu cha elimuy a krkristo na majadiliano kati ya imani ya Kikristo na falsafa ya Kigiriki.
 
Aleksandria ilikuwa mji mkuu wa Misri. Kabla ya kutwaliwa kwa Misri na [[Dola la Roma]] wafalme Waptolemayo wa Misri waliwahi kuunda maktaba maarufu ambayo huaminiwa kuwa wakati wake ilikuwa maktaba kubwa duniani yenye vitabu 700,000. Kwa hakika ilikuwa maktaba kubwa kote Afrika, Ulaya na Asia ya Magharibi. Hii ilikuwa na thamani kubwa kupita kiasi wakati ambako vitabu viliandikwa na kunakiliwa kwa mkono tu hivyo kuwa haba. Aleksandria ilikuwa kitovu cha elimu na uchunguzi wa kitaalamu duniani.
 
Mwalimu wake wa kwanza anayejulikana alikuwa [[Panteno]]. Tangu mnamo 200 [[Klemens wa Aleksandria]] alichukua uongozi aliyefuatwa na [[Origene]] na wataalamu wengine wanaoheshimiwa kama watakatifu katika kanisa la orthodoksi na kanisa katoliki.
 
Chuo kikastawi mwanzoni katika vipindi ambako Wakristo hawakuteswa katika Misri kikaona matatizo mazoto wakati wa madhulumu. Tangu 311 uhuru wa kidini kilitangazwa na [[Kaisari]] [[Konstantino Mkuu]] katika Dola la Roma na mateso ya Wakristo yalikwisha. Chuo cha Aleksandria kikaendelea kutembelewa na wataalamu Wakristo kutoka pande zote za nchi za Mediteranea.
 
[[category:Misri]]
[[Category:Historia ya Kanisa]]
[[Category:Teolojia]]