Binadamu : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
viungo vya nje Tags: Hariri ya simu Hariri ya wavuti ya rununu |
d Masahihisho aliyefanya JOSUE KAMARA (Majadiliano) yalirejeshwa hadi sahihisho la mwisho na Riccardo Riccioni Tag: Rollback |
||
Mstari 43:
Hatimaye, katika [[karne ya 20]] watu walikwenda kukaa kwa muda katika bara la [[Antaktika]] kwa ajili ya utafiti.
== Upekee wake ==
Ingawa binadamu ana undugu mkubwa wa kibiolojia na [[sokwe]] na viumbe vingine, ustawi wake hauna mfano, kiasi cha kufanya wengi waamini tofauti iliyopo inadai kuelezwa kwa uwemo wa [[roho]] ndani ya [[mwili]] wake; roho ambayo [[dini]] hizo [[imani|zinasadiki]] imetiwa na [[Mungu]] moja kwa moja.
== Binadamu kadiri ya Biblia ==
Kadiri ya [[Biblia]], binadamu ameumbwa “kwa mfano wa Mungu” ([[Mwa]] 1:27), mwenye [[roho]] isiyokufa. Hivyo, Mungu amependa kuwasiliana na watu, akijitambulisha na kujitoa kwetu, tuweze kuishi katika [[urafiki]] naye na hatimaye tushiriki [[heri]] yake.
Ameshirikishwa naye ukuu juu ya viumbe vyote vinavyoonekana. “Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizoziratibisha; mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshima” ([[Zab]] 8:3-5). “Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu” ([[Yoh]] 15:15). Amefanya hivyo kwa maneno na matendo yanayoshikamana sana kwa kuwa maneno yanafafanua matendo, nayo matendo yanathibitisha maneno.
Mungu ametufunulia pia [[ukweli]] juu yetu wenyewe akijibu kabisa maswali yanayotusumbua kuhusu [[Maana ya maisha|maana]] na lengo la [[maisha]] yetu. “Mungu hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli” ([[1Tim]] 2:4). “Mungu si mtu, aseme uongo” ([[Hes]] 23:19). Yeye hadanganyiki wala hadanganyi.
Kati ya viumbe vinavyoonekana, mtu tu ni [[nafsi]], akiwa na uwezo wa kujifahamu, kujitawala, kujitolea na kupendana na wengine. Basi, anapaswa kulinda hadhi hiyo asitawaliwe na [[tamaa]] za kila aina. Akifanya hivyo anatimiza mpango wa [[Mungu]] juu yake na kupendana naye.
[[Malaika]] na watu ndio viumbe pekee vyenye hiari ya kuchagua wenyewe wachangie mpango wa Mungu au la. “Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi, chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako” ([[Kumb]] 30:19-20).
Malaika na watu wanaweza kuchagua hata wawe wema au wabaya [[milele]]. “Kulikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni” ([[Ufu]] 12:7-8).
Chaguo letu binadamu linafanyika siku kwa siku kwa kuchukua misimamo mizuri au mipotovu kuhusu [[dini]] na [[maadili]]. “Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima” ([[Yoh]] 5:39-40).
Binadamu ni [[umoja]] wa mambo mawili: roho iliyoumbwa na Mungu moja kwa moja, na [[mwili]] ulioumbwa naye kwa njia ya [[wazazi]]. [[Maumbile]] hayo yanatakiwa kukamilika kwa kupokea na kutimiza [[upendo]] wa Mungu aliyesema, “’Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi’. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba” ([[Mwa]] 1:26-27).
Hivyo, mwili wetu ni muhimu, kwa sababu umeumbwa na Mungu, umetwaliwa na [[Mungu Mwana|Mwanae]] ili atuokoe, umehuishwa na [[Roho Mtakatifu]] atakayeutukuza siku ya [[Ufufuko|ufufuo]] kwa mfano wa Yesu. “Mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake. Je, hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye?… Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu?” ([[1Kor]] 6:13-16,19).
[[Utoto]]ni anasukumwa tu na [[haja]] za [[umbile]] lake, ambazo ni muhimu kwake na anazilenga bila ya kuhitaji juhudi.
Lakini akikua anaanza kutambua [[tunu]] za [[maadili]] na [[dini]], ambazo ni njema, ni muhimu kwa zenyewe na zinamdai azifuate kwa nia imara hadi afikie lengo.
Kwa bidii za kudumu za namna hiyo anamlenga hasa Mungu, wema mkuu.
Anapopitia misukosuko ya [[ujana]] asikubali kushindwa na [[vionjo]] wala asikate tamaa, kwa kuwa Mungu amemuumba atawale hata nafsi yake na [[mwili]] wake.
Mtu wa kwanza kuumbwa na Mungu kadiri ya Biblia alikuwa Adamu, akifuatwa na [[Eva]] [[Mke|mkewe]]. Hapo “Mungu aliona kila kitu alichokifanya, na tazama ni chema sana” (Mwa 1:31).
Hata hivyo, baada ya [[dhambi ya asili]] anadaiwa bidii katika kutekeleza tunu ili wema alionao uzae matunda.
Basi, apanie kukuza wema aliojaliwa ili kesho awe mtu bora kama [[mzazi]], [[raia]], kiongozi wa dini na [[jamii]] n.k.
Penye nia pana njia hata ya kuelekea [[utakatifu]] utakaokamilika katika [[uzima wa milele]].
Binadamu amekabidhiwa na Mungu [[dunia]], lakini hasa amekabidhiwa nafsi yake mwenyewe. Itamfaa nini kujua na kutawala [[ulimwengu]], asipojijua na kujitawala kweli?
== Binadamu na elimunafsia ==
Line 74 ⟶ 97:
* [[Mtu wa kwanza alitoka wapi]]
==Tanbihi==
{{marejeo}}
Viungo vya nje▼
* [http://binadamu.net]
{{Sokwe}}
[[Jamii:Jamii]]
[[Jamii:Binadamu]]
[[Jamii:Binadamu na jamaa]]
[[Jamii:Biolojia]]
[[Jamii:Saikolojia]]
[[Jamii:Biblia]]
|