Galaksi : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 5:
Kuna galaksi nyingi sana [[ulimwengu]]ni. Kwa [[wastani]] kila galaksi imekadiriwa kuwa na nyota kama [[bilioni]] 100 lakini kuna galaksi kubwa na ndogo.
Galaksi yetu, ikiwemo [[mfumo wa jua|mfumo wetu wa jua]], imekadiriwa kuwa na nyota zaidi ya 300,000,000,000. Sehemu ya nyota hizi zinaonekana kama [[kanda]] la kung'aa kwenye [[anga]] la [[usiku]] linalojulikana kwa [[rangi]] yake kama [[njia nyeupe]] au "njia ya [[maziwa]]"<ref>Maziwa (mfano maziwa ya ng'ombe) kwa [[Kigiriki]] huitwa "galaks" na hapo aili ya jina "galaksi".</ref>. Umbo lake linafanana na kisahani kikiwa na [[kipenyo]] cha [[mwakanuru|miakanuru]] 100,000 na kikiwa na [[unene]] wa
Kwenye kitovu cha galaksi graviti ni kubwa sana kiasa cha kwamba galaksi nyingi huaminiwa kuwa na [[shimo jeusi]] kituvoni<ref>[https://www.nrao.edu/pr/2005/sagastar/ Astronomers Get Closest Look Yet At Milky Way's Mysterious Core], tovuti ya National Radio Astronomy Observatory, Marekani, iliangaliwa Machi 2019 </ref>.
Galaksi zilizo karibu angani zinaitwa [[Mawingu ya Magellan]] ambayo ni galaksi mbili ndogo zilizopo kwenye umbali wa miakanuru 170,000 na 200,000. Galaksi kubwa ya jirani ni [[Andromeda (galaksi)|Andromeda]] na ina umbali wa miakanuru milioni 2.5.
[[Idadi]] kamili ya galaksi zote angani haijulikani. Kuna makadirio ya kwamba idadi ya galaksi zinazoweza kuangaliwa kwa vyombo vinavyopatikana ni mabilioni. Hadi sasa sehemu ndogo tu imehesabiwa lakini mara kwa mara galaksi mpya zinatambuliwa kwa njia ya [[darubini]] au vyombo vya angani.
Line 13 ⟶ 15:
Galaksi zinazojulikana zimepewa namba katika orodha ya kimataifa na [[wanasayansi]] wa [[astronomia]].
Galaksi kati yao hujumuika pia zikiathiriana kwa njia ya [[graviti]] yao na kuzunguka kitovu cha graviti cha pamoja. Galaksi hadi 50 zinazoshikamana katika [[kipenyo]] cha [[miakanuru]] milioni 10 huitwa [[kundi la galaksi]] (ing. ''galaxy group''). Kuna pia galaksi mamia hadi maelfu kadhaa zinazoshikamana na hii huitwa [[fundo la galaksi]] (ing. ''galaxy cluster'')
==Marejeo==
|