Dajaja (kundinyota) : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
No edit summary
Mstari 6:
 
==Jina==
Dajaja (Cygnus) ilijulikana kwa mabaharia Waswahili tangu miaka mingi wakifuata njia yao baharini wakati wa usiku kwa msaada wa nyota. Walipokea jina hili kutoka kwa Waarabu wanaosema <big>الدجاجة</big> ''al-dajaja'' wakimtaja ndege wa aina ya [[kuku]]. <ref>ling. Knappert 1993</ref>. Waarabu walipokea jina hili kutoka kwa [[Klaudio Ptolemaio|Ptolemaio]] aliyeiita Ορνις ''ornis'' yaani ndege au kuku<ref>Kwa Kigiriki cha Kale neno Ορνις ''ornis'' iliweza kumaanisha ndege kwa jumla au pia kuku kwa maana ya pekee. Linganisha Paul Kunitzsch, Almagest uk.179</ref>. Wagiriki wa Kale kwa jumla waliona hapa ndege waliotaja kwa majina tofauti<ref>Allen uk 192 anataja Ornis kama jina la kawaida; ni [[Eratosthenes]] aliyewahi kutumia jina “kyknos”. Allen anaona Wagiriki walipokea kundinyota hiihili kutoka kwa Wababeli bila kukumbuka hao walimaanisha ndege gani.</ref> .
 
Katika mapokeo ya baadaye hasa wakati wa Kiroma ndege ilichukuliwa kumaanisha [[bata-maji]] au “kyknos” ([[lat.]] Cygnus) iliyounganishwa na ndege huyu wa angani kati ya Wagiriki na [[Waroma wa Kale]]. Katika [[mitholojia ya Kigiriki]] "''kyknos''"inaweza kurejelea masimulizi ya mungu mkuu [[Zeus]] aliyechukua umbo la bata maji akitembea duniani na kutafuta mapenzi na mabinti wa kibinadamu<ref>Linganisha mitholojia yala kundinyota [[Jauza (kundinyota)|Jauza]]!</ref>. Kwa mapokeo tofauti jina la “kyknos” linarejelea masimulizi ya mungu Phaeton aliyekuwa mwana wa [[Helios]] mungu wa jua. Phaeton aliwahi kuendesha gari la jua la babaye angani kwa kasi kubwa mno akasababisha hatari ya kuchomwa kwa mbingu na Dunia. Hapo baba wa miungu Zeus alipaswa kurusha radi dhidi ya gari la jua na kumwua Phaeton. Phaeton akaanguka chini katika mto Nahari (Eridanus) na kwa muda mrefu rafiki yake Kyknos alitafuta mifupa yake katika vilindi vya mto ili aweze kumpatia mazishi halisi. Miugu kwa jumla waliguswa na upendo alionyesha wakamgeuza kuwa kyknos = bata-maji na kumweka angani kati ya nyota. Kwa hiyo Waarabu walitumia hapa jina la kale zaidi la Wagiriki kwa kundinyota hiihili. Katika mapokeo ya kimagharibi kuna pia mifano ambako “Gallina” (=Kuku) ilitumiwa badala ya Cygnus hadi karne ya 18.<ref>Allen uk. 194 </ref>.
 
Cygnus - Dajaja ni kati ya makundinyota yaliyotajwa tayari na [[Klaudio Ptolemaio]] (kwake kama ornis - ndege) katika karne ya 2 BK. Iko pia katika orodha ya makundinyota 88 ya [[Umoja wa Kimataifa wa Astronomia]] <ref>[https://www.iau.org/public/themes/constellations/ The Constellations], tovuti ya International Astronomical Union , iliangaliwa Julai 2017</ref> kwa jina la Cygnus. Kifupi chake rasmi kufuatana na [[UKIA]] ni 'Cyg'.<ref name="pa30_469">{{cite journal | last=Russell | first=Henry Norris | title=The New International Symbols for the Constellations | journal=[[Popular Astronomy (US magazine)|Popular Astronomy]] | volume=30 | pages=469–71 | bibcode=1922PA.....30..469R | year=1922}}</ref>