Nyasa (ziwa) : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
→‎Eneo la Ziwa: sheria ya kimataifa
Mstari 22:
Baada ya mwaka [[1919]] [[Uingereza]] ilitawala [[Tanganyika]] pamoja na [[Malawi]] (Nyassaland), hivyo hakukuwa na shida.
 
Kabla ya uhuru, wakati wawakilishi wa TANU walichaguliwa tayari kuwa wabunge katika bunge la kikoloni (legislative council) na Julius Nyerere alikuwa waziri mkuu wa Tanganyika tangu 1960, mbunge Chifu Mhaiki alitaka serikali iangalie upya haki za Tanganyika kwa maji ya ziwa. Wakati ule waziri mkuu Nyerere alijibu: "Tunajua kwamba hakuna tone la maji kwenye Ziwa Nyasa ni mali ya Tanganyika kufuatana na mapatano haya. Hali halisi tungedai serikali jirani ibadilishe mipaka kwa manufaa ya Tanganyika." <ref>"We know that not a drop of the water of Lake Nyasa belongs to Tanganyika under the terms of the agreement, so that in actual fact we would be asking a neighboring Government [to] change the boundary in favor of Tanganyika.", Tanganyika Legislative Council, Official Report uk 614-615, kufuatana na Maluwa uk. 372</ref>. Chifu Mhaiki alirudia swali lake alipokuwa mbunge katika Bunge la Kitaifa baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1962 na safari hii waziri mkuu Rashidi Kawawa alijibu tena kwamba hakuna sehemu ya Ziwa Nyasa iliyokuwa ndani ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, kwamba Uingereza kaijubadilisha mipaka hii na kwamba hata kama kuna hasara kwa Tanganyika serikali haiwezi kuanza majadiliano juu ya swali hili na Uingereza au serikali ya Nyasaland kabla ya uhuru wa nchi hii jirani<ref>Maluwa, uk. 373</ref>.
Kumbe, baada ya [[uhuru]] Malawi ilitaka kutumia [[historia]] hii kama [[haki]] yake ya kitaifa. [[Polisi]] yake ilijaribu kutawala [[wavuvi]] na [[feri]] za Tanzania ziwani. Mzozo huu ulisababisha [[risasi]] kufyatuliwa.
 
Tarehe 3 Januari 1967 serikali ya Tanzania iliandika mara ya kwanza kwa serikali ya Malawi na kuifahamisha kwamba iliona mpaka baina ya nhci hizi ilifuata mstari wa kati wa Ziwa Nyasa. Malawi ilithibitisha kupokelewa kwa barua hii bila kuijibu rasmi. Hata hivyo rais Banda wa Malawi alikataa madai ya tanzania mbele ya bunge lake. [[Polisi]] ya Malawi ilijaribu kutawala [[wavuvi]] na [[feri]] za Tanzania ziwani. Mzozo huu ulisababisha [[risasi]] kufyatuliwa hadi kutulia mwaka 1968.
 
Hadi leo hakuna mapatano rasmi lakini nchi zote [[mbili]] zinaendelea bila kutumia nguvu. Hali halisi Malawi imeheshimu dai la Tanzania, haijasumbua tena wavuvi wala feri za jirani ndani ya robo ya kaskazini-mashariki ya ziwa.