Sabato : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
No edit summary
d Masahihisho aliyefanya Frank de dfl (Majadiliano) yalirejeshwa hadi sahihisho la mwisho na Magioladitis
Tag: Rollback
Mstari 17:
[[Tabia]] ya pekee ya amri hii ni [[sharti]] la kuwapa hata [[wafanyakazi]] na [[watumwa]] nafasi hii ya kupumzika, hasa inavyotajwa katika [[Kumbukumbu la Torati]] 5:12-15 ambamo sababu si [[uumbaji]] bali [[ukombozi]] ambao Mungu kwa njia ya Musa aliwatoa Waisraeli utumwani [[Misri]]. Hivyo amri hii inatazamwa kama [[sheria]] ya kwanza ya kutunza [[haki za wafanyakazi]].
 
Kadiri ya Kutoka 31:13-17 adhimisho la Sabato lilitolewa na Mungu kwa Waisraeli kama [[ishara]] ya [[agano]] la kudumu kati yake na wao.Nasi kama waizraeel wa kiroho tunapaswa kuiga ama kuufuata mfano huu wa waizrael.kwani MUNGU ametuagiza kufuata maagizo yake .
 
== Mapokeo ya Talmudi ==
Mstari 28:
[[Wayahudi huria]] hawachukui amri hizi vikali vile. Kwa mfano Myahudi huria asingeandika chochote kinachohusika na kazi yake lakini hana shida kuandika [[barua]] isiyo ya kikazi. Atajaribu kuepukana na tendo la kununua kitu [[duka]]ni lakini kama kuna haja atafanya hivyo.
 
Wayahudi wote wafundisha ya kwamba sheria zote za Sabato zaweza kuvunjwa kama [[uhai]] wa [[binadamu]] uko hatarini.ba Sabato
 
== Wakristo na Sabato ==
Katika [[Ukristo]] Sabato imehamishwa na wanadamu kwenda siku ya [[Jumapili]] isipokuwa kati ya [[madhehebu]] madogo kama [[Waadventista Wasabato]].
 
Chanzo cha badiliko hilo kinaonekana katika taarifa ya [[Matendo ya Mitume]] 20:7 inayoonyesha ya kwamba wakati wa [[Mtume Paulo]] Wakristo walikutana siku ya kwanza ya juma. Sababu yake ilikuwa kukumbuka [[ufufuko wa Yesu]] aliyetoka [[kaburi]]ni siku hii ya kwanza yaani Jumapili.Hivyo jumapili sio siku ya sabato bali ji siku ya kufufuka kwa yesu ila siku ya sabato inabaki kuwa jumamosi kama ilivyo andikwa katika biblia.

Agano Jipya halielezi badiliko hili lilitokeaje, lakini linahusianishwa na matukio mawili ya Kanisa katika [[karne ya 1]]: polepole Wakristo wa mataifa waliwapita wale wa Kiyahudi kwa idadi na bidii, nao hawakujali tena mambo mbalimbali ya [[Agano la Kale]]; amani kati ya Wakristo na Wayahudi ilizidi kupungua, na baada ya maangamizi ya [[Hekalu la Yerusalemu]] ([[70]] [[BK]]) hao wa mwisho waliwakataza hao wa kwanza wasiendelee kushiriki ibada zao sinagogini.
 
[[Barua kwa Wakolosai]] 2:16 inawahimiza Wakristo hao wasijisikie kubanwa na masharti ya Kiyahudi wala kusumbuliwa na mtu kuhusu Sabato na siku nyingine za [[kalenda ya Kiyahudi]].