[[Picha:Arbres.jpg|thumb|400px|Miti ikistawi kando ya [[ziwa]].]]
'''Mti''' ni [[mmea]] mkubwa wa kudumu wenye [[shina]] la [[ubao]].
Miti huishi miaka mingi; miti yenye [[umri]] mkubwa imejulikana kuwepo kwa miaka 4,800 huko [[Kalifornia]]. Kuna [[dalili]] za mti mmoja uliopimwa huko [[Uswidi]] kuwa na miaka zaidi ya 9,000.
Kwa jumla [[ugumu]] wa ubao na [[uzito]] wake hutegemea namna ya kukua kwa mti. Miti inayokua polepole huwa na ubao mgumu na mzito zaidi; miti inayokua harakaharaka huwa na ubao mwepesi na laini.