Jinai : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary Tag: 2017 source edit |
No edit summary Tag: 2017 source edit |
||
Mstari 1:
'''Jinai''' ni kitendo kinachofanywa na [[Binadamu|mtu]] ambacho ni kinyume na [[sheria]] za [[nchi]] au eneo. Kwa hiyo jinai inafafanuliwa na [[sheria]] inayotaja matendo maalum kuwa vile.
Matendo yanayotajwa kama jinai hutazamiwa kuwa hatari ya amani katika jamii na pia kuvunja haki za watu. Kwa hiyo katika mifumo ya sheria ya kisasa [[dola]] linalenga kulinda amani na haki kwa kutunga sheria zinazokataza jinai.
Kwa kawaida tendo fulani linahitaji kutendwa pamoja na nia ya kuvunja sheria ili kutajwa jinai. Hata hivyo, pia matendo maalum yanayotendwa "kwa namna ya kutokuwa mwangalifu au kupuuza kwa kiasi cha kuhatarisha maisha ya binadamu au kusababisha dhara kwa mtu mwingine yeyote"<ref>Kanuni ya Adhabu Tanzania (Penal Code , Chapter 16 of the Laws (revised), Jinai kwa kutojali na kupuuza, ss. 233. ([https://sheriakwakiswahili.blogspot.com/p/downloads.html<nowiki> online hapa])</ref> yanaweza kuangaliwa kama jinai.
|