Shairi : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary Tag: Reverted |
d Masahihisho aliyefanya Carren loy (Majadiliano) yalirejeshwa hadi sahihisho la mwisho na Idd ninga Tag: Rollback |
||
Mstari 1:
[[File:Mrisho Mpoto.jpg|thumb|right|Mshairi Mrisho Mpoto akiwa katika Tamasha la [[Filamu]] la Kimataifa la [[Zanzibar]] (ZIFF) 2011]]
'''Shairi''' (kwa [[Kiingereza]]: ''poem'') ni aina ya [[fasihi]]. Mashairi ni [[tungo]] zenye kutumia mapigo ya [[silabi]] kwa utaratibu maalumu wa [[Muziki|kimuziki]] kwa kutumia [[lugha ya mkato]], [[lugha ya picha]] na [[tamathali za semi]].
Mashairi ndiyo fasihi pekee [[duniani]] ambayo huingizwa katika [[fasihi andishi]] na [[fasihi simulizi]].
Mashairi huweza kuandikwa au kutungwa kulingana na jinsi yanavyoonekana. Hii ina maana kuwa, mashairi huweza kutofautishwa kwa [[idadi]] ya [[Mshororo|mishororo]], jinsi [[Neno|maneno]] yalivyopangwa, [[urari]] wa [[kina (fasihi)|vina]] na kadhalika. Mtu anayetunga shairi huitwa [[malenga]]. Mtu anayekariri au kuimba shairi huitwa [[manju]].
Kuna [[mashairi]] yanayofuata taratibu za [[mapokeo|kimapokeo]], yaani yanazingatia taratibu za [[urari]] na vina, [[mizani (ushairi)|mizani]], idadi sawa ya mistari, vituo na [[ubeti|beti]]. Mashairi hayo huwa na mizani 14 au 16 katika kila mstari, yaani mizani 7 au 8 kwa kila kipande cha mstari.
Pia kuna mashairi yasiyofuata utaratibu huo wa kimapokeo na huitwa mashairi ya kimamboleo. Mashairi hayo mara nyingi huwa ni [[nyimbo]].
Mstari 24:
Kuna aina kuu mbili za mashairi, nazo ni kama zifuatavyo:
===(i) Mashairi ya kimapokeo===
Haya ni mashairi yanayozingatia kanuni za muwala/urari (ulinganifu) wa mizani, vina, idadi ya mistari katika kila [[ubeti]] na kituo katika shairi. Vilevile huitwa ''mashairi funge''.
Aina ya mashairi kulingana na mtindo huu wa mapokeo,hupatikana kwa kuangalia idadi ya mishororo katika kila ubeti.
Mstari 40:
==Ubeti==
Ubeti ni fungu la mistari lenye maana kamili. Ubeti unaweza kulinganishwa na [[aya]] katika maandiko ya kinathari. Mara nyingi ubeti huishia katika kituo. Ubeti mmoja unaweza kuwa na:
*Mstari mmoja ([[tamonitha]])
*Mistari miwili (tathiniya/[[tathinia]]/uwili): shairi hili huwa na mishororo miwili katika kila ubeti. vina vyake vyaweza kuwa na mtiririko.
*Mistari mitatu ([[tathilitha]]): shairi hili huwa na mishororo mitatu katika kila ubeti. vina vyake huenda vikawa na urari.
*Mistari mine ([[tarbia]]): shairi la aina hii huwa na mishororo minne katika kila ubeti. mara nyingi shairi hili hugawanywa katika sehemu mbili, [[ukwapi na utao]]. Mshororo wa kwanza wa shairi hili huitwa kipokeo, wa pili huitwa mloto, wa nne huitwa kibwagizo. kibwagizo huwa kinarudiwarudiwa katika kila ubeti.
*Mistari mitano ([[takhmisa]]): hili ni shairi lenye mishororo mitano katika kila ubeti
*Mistari zaidi ya mitano ([[sabilia]]), kwa mfano: [[tasdisa]] huwa na mishororo sita katika kila ubeti, [[tathmina]] huwa na mishororo minane katika kila ubeti, [[ukumi]] huna na mishororo kumi katika kila ubeti.
==Aina za mashairi jinsi yanavyojitokeza==
Mstari 53:
==Kituo==
Ni mstari (mshororo) wa mwisho katika kila ubeti wa shairi ambao huonesha msisitizo wa ubeti mzima au shairi zima. Wakati mwingine kituo huitwa
Kibwagizo ni mshororo wa mwisho katika ubeti ambao unajirudiarudia.
|