'''Zohali''' (kutoka [[kar.]] [[:ar:زحل|زحل]] ''(zuhalzuḥal)'', pia: '''Zohari''' <ref>Katika vitabu kadhaa sayari hii inaitwa Sarateni, Satani au Saratani; lakini Saratani ni jina la kundinyota linalojulikana pia kama "Cancer"; mchanganyiko unatokana na matamshi mabaya ya jina la Kiingereza "Saturn". Linganisha orodha ya [[Jan Knappert]] kuhusu majina ya nyota, sayari na kundinyota (angalia makala ya Knappert)</ref> kutoka [[Kilatini]]/[[Kiing.]] [[w:Saturnus|Saturnus]]) ni [[sayari]] ya sita toka kwenye [[jua]] katika [[Mfumo wa Jua]]. Ni sayari kubwa ya pili baada ya [[Mshtarii]].
Inaonekana kwa macho matupu si lazima kutumia darubini. Kwa hiyo imeshajulikana tangu zamani ilitambuliwa na wataalamu wa nyakati za kale.