'''Chawa''' ni [[wadudu]] wadogo wa [[oda]] ndogo [[Phthiraptera]] katika nusungeli[[nusuoda]] [[PterygotaTroctomorpha]] (wenyewa [[bawa|mabawaoda]]),lakini[[Psocodea]]. hata kama wahengaWahenga wao walikuwani [[chawa-vitabu]] na mabawa,kama hawa chawa hawanayohawana mabawa. Wadudu hawa wote ni [[kidusia|vidusia]] wa nje juu ya [[ndege (biolojia)|ndege]] na [[mamalia]] isipokuwa [[Monotremata]] ([[kinyamadege]] na [[mhanganungu]]), [[popo]], [[nyangumi]], [[pomboo]] na [[kakakuona]]. Kuna aina mbili za chawa: wanaokula [[nywele]], [[manyoya]] na [[seli]] za [[ngozi]] zilizokufa, na wanaofyunza [[damu]] ya mwenyeji. Chawa wa aina ya kwanza wana vipande vya mdomo vya kutafuna, wale wengine wana mdomo wa kufyunza. Miguu inabeba aina za magando madogo ili kushika nywele au manyoya ya mwenyeji. Kwa kawaida [[yai|mayai]] ya chawa yamegandia nywele au manyoya, au pengine yamewekwa ndani ya shina la unyoya.