Vina vya kati ni "ni" navyo vya mwisho ni "ia" katika kila mshororo.
Shari ni Mafi
==Ubeti==
Ubeti ni fungu la mistari lenye maana kamili. Ubeti unaweza kulinganishwa na [[aya]] katika maandiko ya kinathari. Mara nyingi ubeti huishia katika kituo. Ubeti mmoja unaweza kuwa na:
kama wewe
*Mstari mmoja ([[tamonitha]])
*Mistari miwili (tathiniya/[[tathinia]]/uwili): shairi hili huwa na mishororo miwili katika kila ubeti. vina vyake vyaweza kuwa na mtiririko.
*Mistari mitatu ([[tathilitha]]): shairi hili huwa na mishororo mitatu katika kila ubeti. vina vyake huenda vikawa na urari.
*Mistari mine ([[tarbia]]): shairi la aina hii huwa na mishororo minne katika kila ubeti. mara nyingi shairi hili hugawanywa katika sehemu mbili, [[ukwapi na utao]]. Mshororo wa kwanza wa shairi hili huitwa kipokeo, wa pili huitwa mloto,wa tatu huitwa mleo, wa nne huitwa kibwagizo. kibwagizo huwa kinarudiwarudiwa katika kila ubeti.
*Mistari mitano ([[takhmisa]]): hili ni shairi lenye mishororo mitano katika kila ubeti
*Mistari zaidi ya mitano ([[sabilia]]), kwa mfano: [[tasdisa]] huwa na mishororo sita katika kila ubeti, [[tathmina]] huwa na mishororo minane katika kila ubeti, [[ukumi]] huna na mishororo kumi katika kila ubeti.