Udikteta : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary Tags: Mobile edit Mobile web edit |
No edit summary |
||
Mstari 1:
[[Picha:Benito Mussolini and Adolf Hitler.jpg|thumb|200px|[[Benito Mussolini]] na [[Adolf Hitler]] walikuwa madikteta wa [[Italia]] na [[Ujerumani]] waliofuata mfumo wa [[ufashisti]] hadi waliposhindwa katika [[Vita vikuu vya pili]].]]
[[Picha:S Abacha.jpg|thumb|200px|[[Sani Abacha]] alikuwa [[dikteta wa kijeshi]] wa [[Nigeria]] miaka [[1993]] hadi [[1998]].]]
'''Udikteta''' (kutoka [[neno]] lenye [[asili]] ya [[Kilatini]]: ''dictator''; pia: '''imla''' kutoka [[Kiarabu]]) ni [[mfumo]] wa [[utawala]] wa nchi ambapo [[mtu]] mmoja asiyebanwa na [[sheria]] wala [[katiba]] anashika [[madaraka]] ya [[serikali]] na ana uwezo wa kuyatumia jinsi anavyoamua mwenyewe.
== Udikteta wa mtu mmoja au wa kundi ==
Mtu huyu anaitwa "[[dikteta]]" ingawa [[cheo]] rasmi mara nyingi ni "[[rais]]" au "kiongozi wa taifa". Wakati mwingine neno "udikteta"
Aina nyingine ni [[udikteta wa chama]]. Mfano wa [[historia|kihistoria]] ulikuwa udikteta wa [[chama cha kikomunisti]] katika [[Urusi]], [[China]] na nchi zilizofungamana nazo. Mfano mwingine ni mfumo wa [[ufashisti]] katika [[Italia]] na [[Ujerumani]] hadi [[mwaka]] [[1945]].
== Ufalme na udikteta ==
Katika historia mfumo wa [[ufalme]]
== Udikteta wa kijeshi ==
Aina ya udikteta inayotokea mara kadhaa [[duniani]] ni udikteta wa kijeshi ambao [[Kiongozi|viongozi]] wa jeshi wamechukua madaraka ya serikali kwa nguvu ya [[silaha]] zao. Hii ilikuwa njia hasa ya udikteta kuenea [[Afrika]] baada ya [[uhuru]] kwa sababu katika nchi nyingi za Afrika wanajeshi walipindua serikali na kutwaa madaraka kwa [[muda]] fulani.
== Tabia za udikteta ==
=== Sheria na
Kila nchi inahitaji [[sheria]] na pia udikteta hauwezi kuongoza bila sheria. Lakini [[tabia]] muhimu ya udikteta ni ya kwamba dikteta ana nafasi au uwezo wa kupuuza sheria au kufanya maazimio nje ya sheria na hakuna njia ya kumlazimisha kutii sheria.
Mara nyingi uhuru na [[haki]] za wananchi
[[Polisi]] inapewa nafasi ya kuwatesa watu na hii ni aina ya [[adhabu]] bila sheria wala mahakama. Mara nyingi polisi zinapewa pia nafasi ya kuua watu hovyo au kuwafunga
=== Uchaguzi bandia ===
Utaratibu wa [[uchaguzi]] huru haufuatwi. Katika nchi kadhaa uchaguzi hufutwa kabisa kwa miaka mingi. Lakini mara nyingi kuna uchaguzi bandia badala ya uchaguzi huru. Kati ya njia mbalimbali za kuathiri matokeo ya uchaguzi ni:
* kuteuliwa kwa wagombea na serikali na kukataliwa kwa wote ambao serikali haipendezwi nao.
* [[mfumo wa chama kimoja]]
* kutawala usimamizi wa uchaguzi na kutangaza matokeo kufuatana na mipango ya uongozi, si kutokana na [[kura]] zake ama uchaguzi hautokei au serikali inateua wagombea ikiondoa wapinzani wote au uchaguzi unaamuliwa awali na serikali ya kidikteta.
=== Uhuru wa maoni ===
Uhuru wa maoni unabanwa au hata kupigwa marufuku kabisa. Serikali inasimamia [[vyombo vya habari]] kama [[Gazeti|magazeti]], [[redio]] na [[televisheni]]. Kutolewa kwa maoni yasiyopendwa na serikali ni
Jambo la kawaida ni uteuzi wa habari zitakazoonekana kwenye vyombo vya habari. Nchi kadhaa zinajaribu pia kukataza habari za nje kufika. Katika [[Ujerumani ya Mashariki]] kwa miaka kadhaa [[antena]] za TV zilizoelekea [[magharibi]] zilipigwa marufuku kwa sababu serikali ilitaka kuzuia upatikanaji wa TV ya [[Ujerumani ya Magharibi]]. Katika [[Korea ya Kaskazini]] wananchi wa kawaida hawana nafasi ya kuangalia [[intaneti]]. [[Jamhuri ya Watu wa China|China]] inatumia mitambo mingi inayojaribu kuzuia habari fulani kupitia intaneti; kuna [[Maunzilaini|programu]] ambazo zinazuia kuangalia kurasa zenye [[jina]] la “[[Dalai Lama]]” anayehofiwa kama mpinzani wa serikali.
==Viungo vya nje==
|