Mjao : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
New page: '''Mjao''' inaeleza ukubwa wa gimba la hisabati (mchemraba, tufe, mcheduara) kwa kupima nafasi ya yaliyomo yake. Hupimwa katika vizio vya ujazo kama mita ujazo (m³) au [[s... |
(Hakuna tofauti)
|
Pitio la 07:26, 9 Septemba 2008
Mjao inaeleza ukubwa wa gimba la hisabati (mchemraba, tufe, mcheduara) kwa kupima nafasi ya yaliyomo yake. Hupimwa katika vizio vya ujazo kama mita ujazo (m³) au sentimita ujazo (cm³). Kila gimba lenye urefu, upana na kimo huwa na mjao.
Alama yake ni V.
Hali halisi nje ya hisabati kuna njia mbili za kuangalia mjao wa gimba:
- ujazo wa nje kwa jumla (kwa mfano kama kitu kinazamwa katika kiowevu kinasukuma kiasi gani cha kiowevu hiki?)
- ujazo wa ndani (kwa mfano yaliyomo ya boksi au tangi)
Mifano ya kukadiria mjao wa magimba kadhaa
Kadirio ya mjao ni Urefu x Upana x Kimo.
mchemraba mwenye urefu wa ukingo "a":
mchemstatili mwenye urefu wa kingo "a", "b" na "c":
tufe lenye rediasi "r"::
mcheduara au mche mwenye eneo la kitako "A" na kimo "h":