Migoli : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 1:
'''Migoli''' ni [[mji mdogo]] wa [[Mkoa wa Iringa]] nchini [[Tanzania]], kwenye mita 700 juu ya usawa wa bahari.
Unapatikana kando ya [[Bwawa la Mtera]] ambako wakazi wengi hutegemeza maisha yao katika [[uvuvi]].
Eneo hili lina [[rutuba]] lakini [[mvua]] ni chache (kwa kawaida haifikii mm. 300 kwa mwaka), hivyo wakazi hawajishughulishi sana na kilimo, hivyo wananunua nafaka kutoka sehemu ambazo zinalimwa kwa wingi, kama vile [[Ismani]] tarafani na Mtamba Dodoma.
Kumbe ni eneo maarufu kwa [[ufugaji]], hasa wa [[ng'ombe]] na [[mbuzi]], wanaostawi katika mbuga isiyo na [[malale]].
Eneo hili, ambapo inapita barabara kuu ya [[Afrika]] kutoka [[Misri]] hadi [[Afrika Kusini]] (ingawa sehemu hii kati ya [[Dodoma]] na [[Iringa]] haijatiwa lami), ni endelevu hasa ukilinganishwa na vijiji vingine vya nchi ya Tanzania, kwa kuwa una huduma nyingi za jamii ambazo zimetokana na juhudi za [[serikali]] na wananchi wenyewe.
Wafadhili wa miradi mbalimbali ni kama vile [[parokia]] [[Kanisa Katoliki|katoliki]] ya Migoli na makampuni ya mawasiliano kama vile Zain, Tigo, Vodacom na Zantel.
[[Jamii:Mkoa wa Iringa]]
|