Hamshahri : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Created page with '{{Infobox gazo | jina = Hamshahri | jina la gazeti = Hamshahri | picha = | aina = *. Gazeti la kila siku<br> *. Gazeti katika lugha ya Kiajemi | lilianzishwa = | eneo ...'
(Hakuna tofauti)

Pitio la 16:58, 29 Januari 2010

{{Infobox gazo | jina = Hamshahri | jina la gazeti = Hamshahri | picha = | aina = *. Gazeti la kila siku
*. Gazeti katika lugha ya Kiajemi | lilianzishwa = | eneo = Iran | mwanzilishi = Gholamhossein Karbaschi | nchi = [[Iran] | mhariri = | mmiliki = | makaomakuu = Tehran | mchapishaji = Manispaa ya Tehran | usambazaji = 400,000 kila siku | lilikwisha = | machapisho = | tovuti = http://hamshahrionline.ir/ }}

Kuhusu

Hamshahri ni gazeti kuu la kitaifa la Iran katika lugha ya Kiajemi linalochapishwa na Manispaa ya Tehran, na lilianzishwa na Gholamhossein Karbaschi. Hili ndilo gazeti ,la kila siku, la kwanza la Iran linalochapishwa katika rangi zote mbalimbali. Lina kurasa 60 za matangazo na bei yake ni riali 1000 za Iran. Hivi sasa, gazeti hili lina usambazaji wake katika maeneo ya manispaa ya Tehran. Usambazaji wake wa kila ni nakala 400,000 kila siku, huu ni sawa na usambazaji wa magazeti makuu ya Marekani kama San Francisco Chronicle, Boston Globe na Chicago Tribune. [3] Toleo la gazeti hili linaweza kupatikana katika tovuti yake ya hamshahrionline.ir

Hamshahri na Uchaguzi wa Khatami

Katika mwaka wa 1997 wa uchaguzi wa rais nchini Iran, gazeti la Hamshahri, lililoendeshwa wakati huo na Meya wa Tehran,Gholamhossein Karbaschi, lilishitakiwa na wahafidhina kuwa linaunga Khatami. Hii ilionekana kuwa haramu kwa sababu gazeti ambalo linapata ruzuku ya serikali haikukubalishwa kuchukua upande wowote katika uchaguzi. Suala hili ,hatimaye, lilisababisha Karbaschi kupelekwa kortini na kushtakiwa kwa kesi za kufuja mali na akahukumiwa kufungwa jela. Katika muhula wa pili wa Khatami, korti ikahukumu kuwa gazeti hilo linaweza kusambazwa ndani ya Tehran tu.

Shindano la Kimataifa la Uchoraji Katuni

Mnamo Februari 6 2006, Farid Mortazavi, mhariri wa picha wa Hamshahri, alitangaza Shindano la Kimataifa la Uchoraji Katuni Za Holocaust. Shindano hili lilikuwa ili kukemea lililoita "unafiki wa nchi za Magharibi katika uhuru wa kujieleza" huku Hamshahri likidai kuwa nchi za Magharibi hazifai kujadili mada fulani kuhusu Uyahudi kama vile , vifo vya Holocaust. Shindano hili liliisha tarehe Novemba 1 2006 huku Abdellah Derkaoui, mchoraji katuni wa Moroko, akishinda nafasi ya kwanza.

Kupigwa Marufuku

Gazeti hili liliachishwa kuchapishwa mnamo 23 - 24 Novemba 2009 baada ya kuchapisha picha ya hekalu ya Dini iliyopigwa marufuku ya Bahá'í.

Angalia Pia

Virejeleo

  1. ^ "Iran's liberal press tiptoes between "red lines"". Juni 11, 2007. .
  2. ^ "Iran Shuts Newspaper For Publishing Baha'i Temple Photo"
  3. ^ Hafezi, Parisa; Jaseb, Hossein; Mostafavi, Ramin (Novemba 24, 2009). Ban on Iran paper over Baha'i photo lifted. Reuters.
  4. ^ In Iran, ban on popular Hamshahri daily lifted.Press TV. Novemba 24, 2009


Viungo vya nje