Hamas : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 5:
Baada ya uchaguzi migogoro iliendelea kati ya Hamas na serikali ya Palestina, baada ya vita vya Gaza vya 2007 Hamas iliendelea kutawala Gaza na serikali ya Palestina iliwafukuza wabunge wa Hamas kutoka sehemu ya West Bank. Misri na Israeli zilifunga mipaka yake na Gaza na kuzuia kuingia na kutoka kwa watu na bidhaa. JUni 2008, Hamas ilisitisha mashambulizi yake ya roketi dhidi ya Israel baada ya makubaliano na Misri ya kusitisha mapigano.Licha ya makubaliano hayo mashirika mengine yaliendelea na mashambulizi dhidi ya Israeli. Miezi miwili kabla ya mwisho wa kusitisha mapigano ya miezi sita vita ilienea, baada ya wanajeshi wa Israeli kuwaua wapiganaji 7 wa Hamas katika mwezi wa Novemba 4.Mauaji haya yalianzisha upya mashambulizi ya roketi toka kwa Hamas. Israeli ilishambulia Gaza mwisho wa mwezi wa Desemba 2008. mashambulizi ya Israeli yaliendelea mpaka Januari 2009. Baada ya mashmabulizi hayo Israeli walifunga mipaka ya Gaza.
Katika mkataba wa 1988, Hamas linataka kuondoa jimbo la Israeli na kutengeneza jumuiya ya kiislamu ya Kipalestina katika sehemu ambalo sasa ni Israeli, Gaza na West Bank. Hata hivyo katika Julai 2009, Khalid Meshaal ambaye ni mmoja wa viongozi wa Hamas kule Damascus alisema nia ya Hamas ni kushirikiana na Israeli katika "ufumbuzi wa mgogoro wa Waarabu na Israel ambayo ni pamoja na kurudi kwa hali ya Palestina kwa kuzingatia mipaka ya 1967," na pia wakimbizi Wapalestina kupewa haki ya kurudi kwao Israeli na Yerusalemu ya Mashariki kutambuliwa kama mji mkuu wa jimbo jipya la Kipalestina. Mara kwa mara Hamas imesisitiza kuwa mgogoro wake na Israeli ni wa kisiasa na wala si wa kidini lakini baadhi ya waandishi wa habari na makundi ya utetezi wanaamini kwamba mikataba na taarifa kutoka kwa viongozi wa Hamas waliovutiwa na njama nadharia dhidi ya wayahudi.
|