Kuku-mwamba : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
Ukurasa mpya |
(Hakuna tofauti)
|
Pitio la 22:57, 7 Agosti 2010
Kuku-mwamba | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kuku-mwamba shingo-nyeupe
| ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
|
Kuku-mwamba ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Picathartes, jenasi pekee ya familia Picathartidae. Wanatokea misitu ya Afrika chini ya Sahara. Kuku-mwamba wana domo kubwa kama lile la kunguru na kichwa bila manyoya chenye rangi kali (nyeusi na njano au nyekundu). Pia wana rangi ya nyeusi au kijivucheusi juu na nyeupe chini. Shingo yao ni nyeupe au ina rangi ya kijivu. Hula wadudu, kama bungo, mchwa na sisimizi, pia jongoo, tandu, nungunungu, konokono na hata vyura na mijusi. Hulijenga tago lao kwa matope chini ya mwamba. Jike huyataga mayai mawili.
Spishi
- Picathartes gymnocephalus, Kuku-mwamba Shingo-nyeupe (White-necked Picathartes or Rockfowl)
- Picathartes oreas, Kuku-mwamba Shingo-kijivu (Grey-necked Picathartes or Rockfowl)