Antoni Maria Claret : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika 'HISTORIA FUPI YA MTAKATIFU ANTON MARIA CLARET Anton Maria Claret alizaliwa huko Sallent, karibu na Barcelona (Catalonia) mnamo December 23, 1807, ni mtoto wa mten...'
(Hakuna tofauti)

Pitio la 13:46, 3 Novemba 2010

HISTORIA FUPI YA MTAKATIFU ANTON MARIA CLARET

Anton Maria Claret alizaliwa huko Sallent, karibu na Barcelona (Catalonia) mnamo December 23, 1807, ni mtoto wa mtengeneza sufi. Alisoma shule katika kijiji chake (native village), na alipotimiza miaka 12 akawa mfumaji. Baadaye alikwenda Barcelona kuwa mfanyabiashara, na alibaki huko hadi alipotimiza umri wa miaka 20. Hata hivyo, alitenga muda wake kujisomea na kujifunza Kilatini na Kifaransa.

Baada ya kutambua wito wake Mtakatifu katika maisha yake ya dini, aliondoka Barcelona. Alitaka kuwa "Carthusian", lakini alijiunga na Seminay ya Vic, Spain, mwaka 1829, na alitawazwa daraja takatifu la Upadre mnamo June 13, 1835. Alipokea zawadi kutoka Parokia yake, ambako aliendelea kusoma teolojia hadi mwaka 1839; lakini kwa kuwa wito wa kimisionari ulizidi kuwa mkubwa alikwenda Roma. Huko alijiunga na shirika la Majesuit, lakini akaona hajalifurahia kwa maisha yalivyokuwa, hivyo alirudi muda mfupi tu Hispania (Spain) na alifanyakazi ya kichungaji huko Viladrau na Girona, akiwavutia wengi kwa juhudi zake kwa niaba (akiwatetea) ya maskini.

Aliitwa na wakubwa wake huko Vic, na kufanya kazi za kimisionari wakati wote akiwa Catalonia. Mnamo mwaka 1848, alipelekwa Visiwa vya Canary ambako alifanya mafungo kwa miezi 15. Alirudi tena Vic, na kuanzisha Shirika la kimisionari la Watoto wa Moyo Safi wa Maria (Congregation of the Missionary Sons of the Immaculate Heart of Mary) mnamo Julai 16, 1849. Pia alianzisha Maktaba kuu ya Barcelona iliyoitwa "Librería Religiosa" (na sasa inaitwa Librería Claret), na iliyoweza kutoa mamilioni ya nakala kwa kazi nzuri zilizofanywa na Kanisa Katoliki zamani.

Kutokana na kazi yake nzuri, Baba Mtakatifu Papa Pius IX kutokana na maombi ya Malkia Isabella II wa Hispania (queen-regnant Isabella II of Spain) alimtawaza/ alimteua kuwa Askofu Mkuu wa Santiago, Cuba mwaka 1849. Alipofika huko, alianza kazi yake barabara ya mageuzi/ matengenezo katika Seminari ya Santiago, iliyobadilika na kuwa imara na yenye nidhamu. Kwa miaka yake miwili ya kwanza katika utumishi wake huko, zaidi ya ndoa 9,000 nyingi zikiwa za sheria za kimila zilihalalishwa chini ya utamaduni wa Kikatoliki. Alijenga hospitali na shule kadhaa. Katika matukio matatu tofauti, Claret alifanya ziara zenye mpangilio katika jimbo zima, ikiwemo misioni za wenyeji. Mapenzi kwa kazi yake njema kulizua upinzani na wasiopenda maendeleo wa wakati huo, kama ilivyokuwa imetokea kabla huko Uhispania. Si chini ya majribio 15 yalifanywa kwa maisha ya Claret; taya lake liliachanishwa wazi kutoka sikio hadi kidevu kwa kisu cha mauaji huko mashariki mwa jimbo/eneo kuu la Holguin.

Mnamo Februari 1857, aliitwa kwa Malkia Isabella II wa Hispania, na alimfanya kuwa atakuwa akitubu kwake (who made him her confessor). Alipata ruhusa ya kutorudi Cuba tena na aliteuliwa kuwa anakwenda Trajanopolis. Kwa nyongeza alikuwa mshauri wa kiroho wa Malikia, na ndipo mvuto wake ulielekea zaidi katika kuwasaidia maskini na uenezaji wa mafunzo/ elimu (propagate learning); aliishi kwa umakini na uadilifu mkubwa na alilazimika kuwa na makazi ndani ya hospitali huko Italia (yaani wanamolelewa maskini wasiojiweza). Kwa miaka tisa (9) alikuwa mkuu wa seminari (rector) wa Escorial (Escorial monastic school) alikoanzisha maabara ya kisayansi, makumbusho (museum) ya vitu halisi vya kihistoria, maktaba, chuo, na shule za muziki na lugha. Malengo yake ya baadaye yaliharibiwa na Mapinduzi ya mwaka 1868, yaliyohitimisha/ yaliyotupilia mbali utawala wa Malkia Isabella II na hivyo kuanzishwa kwa Jamhuri ya Hispania.

Mnamo mwaka 1869, Claret alirudi tena Roma kuandaa Halmashauri ya Kwanza ya Vatikani (the First Vatican Council). Kutokana na afya yake kutokuwa nzuri, alikwenda Prades Ufaransa, ambako alikuwa bado akisumbuliwa na Wahispania maadaui zake; muda si mrefu baada ya kustaafu kutoka Cistercian abbey huko Fontfroide, Narbonne, kusini mwa Ufaransa, ambako alifariki dunia Oktoba 24, 1870 akiwa na umri wa miaka 63.

Imetayarishwa na kuletwa kwako na: Jasson Charles Kalile (E mail: jassonkalile@gmail.com, Simu: +255 754 380832) KATIBU WA JUMUIYA NDOGONDOGO YA KIKRISTO YA MTAKATIFU ANTON MARIA CLARET, KIGANGO CHA MALAMBA MAWILI, PAROKIA YA MBEZI LOUIS, S.L.P 6813, DAR ES SALAAM. JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM