Pearl Harbor : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 7:
Pearl Harbor ilikuwa maarufu kutokana na mashambulio ya ghafla ya [[Japani]] dhidi ya manowari za Marekani yaliyotokea hapa tar. [[7 Desemba]] [[1941]]. Hatua hii ilisababisha Marekani kuingia katika [[Vita Kuu ya Pili ya Dunia]] na kujiunga rasmi na [[mataifa ya ushirikiano]].
Katika siku kabla ya 7 Desemba wanamaji wa Japani walifaulu kukaribia funguvisiwa na kundi la manowari pamoja na [[manowari ndege]] 6.
Shabaha ya shambulio la Japani ilikuwa kuharibu uwezo wa manowari za Marekani kuingilia katika upanuzi wa mamlaka ya Japani katika Pasifiki hasa kwenye maeneo chini ya utawala wa [[Uingereza]], [[Uholanzi]], [[Ufaransa]] na [[China]]. Lakini shambulio halikugusa kituo cha [[nyambizi]], akiba za fueli, karahana za kijeshi na ofisi za viongozi vya jeshi. Pia manowari ndege zilizokuwa sehemu ya kundi ya Pearl Harbor hazikuharibiwa kwa sababu zote tatu hazikuwepo Hawaii wakati wa shambulio.
|