Metorolojia : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
tahajia
tahajia
Mstari 8:
Metorolojia imeanza kutokea kadri wataalamu walianza kuchukua vipimo halisi vya tabia za angahewa na kuvilinganisha. Mweleko huu ulileta kubuniwa kwa vifaa vya upimaji maalumu.
* vyombo vya kupima kiasi cha [[usimbishaji]] hasa [[mvua]] vilivyosanifishwa na serikali vinajulikana kutoka [[Korea]] mnamo [[1441]]; vilisambazwa kama msaada wa kukadiria kodi za wakulima. Hadi leo kiasi cha mvua kinachonyesha kwa mwezi au mwaka ni kipimo muhimu kwa kupanga shughuli za kilimo.
 
*vyombo vya kupima kasi na mwelekeo wa [[upepo]] kwa mahali fulani vinajulikana tangu [[anemomita]] iliyobuniwa Italia mnamo [[1450]]. Habari hizi ni za kimsingi kwa kuelewa uhusiano kati ya hali ya hewa katima maeneo majirani; ni pia muhimu kwa kupanga kilimo kwa sababu zinatawala sehemu ya [[uvukizaji]] na ni habari za lazima kwa mpangilio wa usafiri kwa [[eropleni]] na pia [[meli]].
 
*Vipimajoto vilivyofanana na vile vya kisasa vilipatikana tangu karne ya 17 na [[1724]] [[Daniel Gabriel Fahrenheit]] alianzsha skeli ya kwanza iliyoruhusu kulinganishwa kwa vipimo vya joto.
 
* Higromita ni kifaa cha kupima kiwango cha unyevu katika hewa na chombo hiki kilibuniwa 1783 na Mfaransa Horace-Bénédict de Saussure.