Moabu : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
nyongeza |
|||
Mstari 2:
[[File:mesha stele.jpg|thumb|[[Jiwe la Mesha]] lilivyopigwa picha mwaka [[1891]] hivi.]]
'''
Zamani eneo hilo lilikuwa [[ufalme]] wa '''Wamoabu'''
Kati ya shuhuda za ki[[akiolojia]] za kabila hilo, muhimu zaidi ni [[Jiwe la Mesha]], linaloeleza ushindi wao dhidi ya mwana wa mfalme [[Omri]] wa [[Israeli]].
Sawa na Isreli Moabu ilikuja chini ya mamlaka kwanza ya [[Ashuru]] na baadaye ya milki ya [[Babeli]]. Mwaka 582 KK mfalme [[Nebukadnezzar II]] wa Babeli alifanya Moabu kuwa sehemu ya milki yake; hivyo ilikuwa sehemu ya ufalme wa [[Uajemi]] baadaye. Wakati wa utawala wa Kiajemi Moabu ilipotea kama taifa la pekee. Makabila ya Waarabu walianza kuingia na kukalia sehemu kubwa za nchi na wakazi waliacha lugha yao wakatumia Kiaramu badala ya lugha yao ya awali.
==Uhusiano kati ya Moabu na Israeli ya Kale==
Kulingana na habari za Biblia uhusiano kati ya Moabu na [[Israeli ya Kale]] mara nyingi haikuwa nzuri wakapigana mara nyingi kivita. Lakini walikuwa karibu katika habari nyingi za jamii na utamaduni wao; lugha yao ilifanana sana na Kiebrania jinsi inavyonoekana kwenye matangazo ya [[jiwe la Mesha]]. Kufuatana na kitabu cha [[Mwanzo (Biblia|Mwanzo]] 19:30-38 walikuwa na ukoo mmoja na wanaisraeli maana Moabu anatajwa kama mjukuu wa [[Abrahamu]] kupitia [[Lutu]] aliyemzaa Moabu na binti yake mkubwa.
Pamoja na masimulizi inayoonyesha uhusiano mbaya kama habari za Bileamu ([[Hesabu (Biblia|Hesabu]] 22-24) au za Egloni na Ehudi ([[Waamuzi (Biblia)|Waamuzi]] 3, 12 ff) kuna pia habari za kinyume. [[Kitabu cha Ruthu]] inasimulia habari za mwanamke wa Moabu anayeendelea kuingia kati ya mababu wa mfalme Daudi.
==Marejeo==
|