Mwerezi : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 1:
'''Mwerezi''' ni [[mti]] wenye [[historia]] katika nchi ya [[Lebanon]].
Historia ya mwerezi wa Lebanon inaanzia miaka mingi nyuma kabla [[Yesu]] [[hajazaliwa, kwa mfano katika [[Zaburi]] 92:12, "Wenye haki watastawi kama mtende]], watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni".
Ni mti unaostahimili hali za [[baridi]] kali na [[joto]] pia.
Mwerezi hukua taratibu sana na hivyo kuufanya kuwa mti wenye [[mbao]] imara. Kwa sababu hiyo mierezi ya Lebanon imekuwa ikikatwa kwa wingi tangu enzi za [[mfalme]] [[Suleiman]] (na wafalme wengine pia) ambaye aliitumia mierezi ya Lebanon katika ujenzi wa [[hekalu la Yerusalemu]].
Mierezi ya Lebanon imekuwa pia ikitumiwa na wenyeji wake kutengenezea [[mashua]] ambazo ziliwawezesha kuwa [[wafanyabiashara]] wa kwanza wa kimataifa.
Kutokana na ukataji uliokithiri, mierezi imekuwa michache sana katika nyakati hizi. Kwa mfano kusini mwa Lebanon ni ngumu hata kuamini kwamba kuliwahi kuwa na misitu yenye miti mikubwa na kuiletea sifa nchi ya Lebanon. Imebaki miti michache katika maeneo ya kaskazini karibu na mpaka wa [[Syria]].
Kutokana na historia iliyotukuka ya mwerezi, mti huo umewekwa katikati ya [[bendera]] ya nchi ya Lebanon na kuwa miongoni mwa alama muhimu za taifa la Lebanon.
[[Jamii:Miti]]
[[Jamii:Mimea ya Biblia]]
[[en:Lebanon Cedar]]
|