Jimbo Katoliki la Musoma : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika ''''Jimbo Katoliki la Musoma''' (kwa Kilatini Dioecesis Musomensis) ni mojawapo kati ya majimbo 34 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania na...'
(Hakuna tofauti)

Pitio la 07:56, 22 Januari 2012

Jimbo Katoliki la Musoma (kwa Kilatini Dioecesis Musomensis) ni mojawapo kati ya majimbo 34 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania na kama hayo yote linafuata mapokeo ya Kiroma.

Eneo lake ni la kilometa mraba 25,150 (Mkoa wa Mara isipokuwa wilaya ya Bunda na parokia mbili katika wilaya ya Bunda vijijini) na lina wakazi 1,040,000, ambao kati yao Wakatoliki ni 215,000 (20.7 %). Parokia ziko 30.

Kikanisa linahusiana na Jimbo Kuu la Mwanza.

Askofu wake ni Michael George Mabuga Msonganzila na makao yake ni Musoma mjini. Kanisa kuu limejengwa kwa heshima ya Mtume Paulo.

Anasaidiwa na mapadri 58, ambao kati yao 38 ni wanajimbo na 20 ni watawa. Kwa wastani kila mmojawao anahudumia waamini 3,707. Pia kuna mabruda 12 na masista 200.

Historia

Uongozi

Viungo vya nje