Kenya People's Union : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Mstari 2:
 
== Historia ==
Mnamo Machi 1966, mzozo ulitokea katika mkutano wa chama tawala KANU uliyofanya mlengo wa kushoto wa chama ukiacha chama hicho na kuanzisha KPU<ref>Bethwell A. Ogot, William Robert Ochieng': [http://books.google.com/books?id=AmFVjigwkxwC&pg=PA98&lpg=PA98&dq=%22Kenya+People%27s+Union%22&source=bl&ots=6RKZc1eFbD&sig=ZJ2D8K_DLQQoGX1YgivmiriRFGM&hl=en&ei=pKriSrfKGIHR-QbogLXeAQ&sa=X&oi=book_result&ct=result&resnum=4&ved=0CBsQ6AEwAw#v=onepage&q=%22Kenya%20People%27s%20Union%22&f=false Decolonization and independence in Kenya]. 1995</ref>. KANU ilibadilisha sheria za uchaguzi kulazimisha wabunge waliyejiunga na KPU kutetea viti vyao katika uchaguzi mdogo. KPU iliweza kushinda hasa kwa [[Waluo]] Mkoani [[Mkoa wa Nyanza|Nyanza]] pekee, huku waliyesimama kwingine wakishindwa na wanasiasa kutoka chama cha KANU ambacho wakati huo kilikuwa kikitawalwa na wanasiasa [[Wakikuyu]] <ref>Abner Cohen: [http://books.google.com/books?id=Mgh7311x8LIC&pg=PA139&dq=kenya+people%27s+union&as_brr=3#v=onepage&q=kenya%20people%27s%20union&f=false Urban Ethnicity]. Routledge, 2004. ISBN 0-415-32982-5</ref>.
Mwisho wa Chama hiki uliwadia wakati wa Ufunguzi wa [[Hospitali ya New Nyanza]] mnamo Oktoba 25, 1969. Wakati huo rais [[Jomo Kenyatta]] hakupendezwa na ufunguzi wa hospitali hiyo kwa vile ilijengwa na fedha za [[Soviet]] na ilionekana kama mradi wa Odinga. Hata hivyo Kenyatta aliongoza sherehe za ufunguzi wake ili kuimarisha umaarufu wake Mkoani Nyanza. [[Wajaluo]] walijulikana kuwa wenye hasira mno kwa kawaida, hasa kwa serikali tangu mauaji ya [[Tom Mboya]] miezi michache iliyotangulia, huku vidole vingi vikimwelekea Kenyatta. Maandamano yalianzishwa wakati wa sherehe hizo za ufunguzi wakati wafuazi wa KPU waliushanbulia msafara wa rais. Zaidi ya watu kumi waliuawa wakati walinzi wa Kenyatta walifunguaufyatuaji wa risasi dhidi ya waandamanaji hao. Odinga na maafisa wengine wa chama cha KPU walititiwa nguvuni siku mbili baada ya tukio hilo. KPU kilifutiliwa mbali mnamo Oktoba 30, 1969, huku [[Kenya]] ikibakia na Chama Kimoja<ref name="incident">Daily Nation, October 23, 2009: [http://www.nation.co.ke/News/politics/-/1064/676220/-/view/printVersion/-/gkqtg1z/-/index.html The incident that transformed Kenya into a de facto one-party state]</ref>.