Tabianchi : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
No edit summary |
||
Mstari 36:
:'''Tabianchi ya msitu wa mvua wa tropiki''': Miezi yote 12 hupatikana na usimbishaji usiopungua milimita 60. Tabianchi hizi hupatikana hasa katika eneo kati ya latitudo za 5 hadi 10 kusini na kaskazini ya [[ikweta]], mahali pachache hata hadi latitudo ya 25° kutoka ikweta. Muda wote kuna kanieneo ya hewa duni kwa hiyo hakuna tofauti ya majira.
:'''Tabianchi ya monsuni ya tropiki''': aina hii ya tabianchi hutokea hasa [[Amerika Kusini]] na katika beseni ya [[Bahari Hindi]] ikisababishwa na upepo wa [[monsuni]] unaobadilika mwelekeo wake kwa utaratibu kimajira. Tabianchi huwa na mwezi kavu zaidi unaotokea mnamo wakati wa [[solistisi]] wa wakati baridi katika nusutufe ya dunia (yaani Desemba kwa nusutufe ya kaskazini na Juni kwa nusutufe ya kusini). Usimbishaji uko chini ya 60 mm/mwezi lakini zaidi ya 100 mm /mwaka.
:[[Tabianchi ya savana]]: inaitwa pia tabianchi ya tropiki nyevu na kavu. Maeneo haya huwa na kipindi cha ukame. Kufuatana na kiasi cha mvua kuna [[savana]] tofauti, ama kavu ama nyevu zaidi. Kiwango cha usimbishaji ni kati ya milimita 500 na 1500 kwa mwaka.
===B: Tabianchi yabisi au nusuyabisi===
Tabia ya kimsingi ya maeneo haya ni kuwa [[uvukizaji]] ni mkubwa kuliko [[usimbishaji]], maana kuna kiasi cha mvua lakini kutokana na joto na jua maji mengi zaidi hupotea kuliko mvua unaonyesha. Kwa hiyo hewa ni kavu.
Kama uvukizaji ni kubwa kuliko usimbishaji kwa muda wa miezi 10-12 kila mwaka tabianchi huitwa yabisi. Hapa kiwango cha mvua hakipitii milimita 80 kwa mwaka.
== Arid ==▼
Kama uvukizaji ni kubwa kuliko usimbishaji kwa muda wa miezi 6 - 9 kila mwaka tabianchi huitwa nusuyabisi.
Tabia ya kawaida kwa eneo yabisi ni kupotea kwa mito ambayo haishii baharini au katika maziwa makubwa bali hupotea tu njiani au kuishia katika maziwa ya chumvi au jangwa la chumvi. Maziwa ya chumvi hupatikana pale ambako maji hayapotei kabisa lakini hupungukiwa mno na mishale ya jua hivyo kiasi kinachobaki kama ziwa au matope huwa na chumvi nyingi. Au hata ziwa la chumvu hukauka kwa miezi mingi ya mwaka na kuacha uwanja mkubwa wa chumvi tu.
Maeneo penye tabianchi yabisi yapo hasa katika sehemu za [[nusutropiki]] zisizofikiwa na upepo wa pasati lakini kuna tabianchi yabisi pia penginepo kwa mfano kwenye milima ya juu au karibu na ncha za dunia.
===C: tabianchi fufutende ya latitudo za kati===
Kanda za tabianchi hii hupatikana kati ya kanda la nusutropiki (lenye halijoto wastani katika mwaka juu ya 20°C) na kanda la baridi (lenye halijoti wastani chini ya 10°C wakati wa mwezi wa joto zaidi).
{{Reflist}}
|