Ibn Battuta : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
d r2.7.3) (Roboti: Imeongeza ba:Ибн Баттута |
Minor fix using AWB |
||
Mstari 2:
'''Abu Abdullah Muhammad Ibn Battuta''' ([[Kar.]]: أبو عبد الله محمد بن بطوطة) alikuwa msafiri, mpelelezi na mtaalamu Mwarabu wa [[karne ya 14]]. Kwa usafiri mgumu wa siku zile alitembelea nchi na kuvuka umbali mkubwa kushinda mtu yeyote wa siku zile anayejulikana. Kutoka kwake tunayo taarifa ya kwanza kuhusu mji wa [[Kilwa Kisiwani]].
Alizaliwa tarehe [[24 Februari]]
Habari zake zimepatikana katika taarifa yake aliyoiandika mwenyewe.
Katika safari yake ya kwanza alikwenda [[Makka]] kupitia [[Misri]], [[Yerusalemu]] na [[Dameski]]. Baada ya kumaliza [[hajj]] akajiunga na msafara kwenda [[Baghdad]] akaona ufalme wa [[Khan wa Il]] na kutembelea [[Uajemi]]kabla ya kurudi Moroko.
Safari yake ya pili ilianza tena kama hajj na safari hii akaendelea kuangalia maeneo ya [[Bahari ya Shamu]] na pwani ya [[Afrika ya Mashariki]]. Akafika hadi [[Kilwa]]kisha akarudi Makka kupitia [[Omani]].
Baada ya kupumzika Makka alikata shauri kuona himaya ya Sultan wa [[Delhi]] ([[Uhindi]]).
Aliamua kujaribu njia kupita [[Uturuki]] kwa sababu alisikia ya kwamba palikuwa na misafara kati ya Waturuki [[Waseldjuki]] na Uhindi. Baada ya kuvuka [[Bahari Nyeusi]] alifika katika milki ya [[Kundi la Dhahabu]] akaendelea katika msafara wa [[Khan]] wa nchi. Alipofika mji mkuu [[Astrakhan]] aliombwa na Khan wa Kundi la Dhahabu mwenyewe kumsindikiza mke wake aliyetaka kutembela nduguye nyumbani kwake [[Konstantinopoli]]. Hivyo Ibn Battuta alifika mara ya kwanza katika nchi nje ya Waislamu.
|