Nyumba ya sanaa Kwenye Makavazi ya Derby : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
d r2.7.1) (Roboti: Imeongeza zh:德比博物馆与艺术画廊
Minor fix using AWB
Mstari 1:
[[File:Derby Museum Flowers 2475926344 d64a8a8f6e o.jpg|right|220px]]
'''Nyumba ya Sanaa Kwenye Makavazi ya Derby''' inayojulikana kwa kiingereza kama '''Derby Museum and Art Gallery''' ilianzishwa mwaka 1879, pamoja na Derby Central Library, katika ujenzi mpya iliyoundwa na Richard Knill Freeman na kutolewa kwa [[Derby]] na Michael Thomas Bass. Mkusanyiko ya vitu vya Sanaa zinazopatikana hapo ni pamoja na nyumba nzima iliyo na picha zilizochorwa na Joseph Wright ya Derby, pia kuna picha kubwa ya Royal Crown Derby na picha zingine za kisanaa kutoka Derby na eneo la jirani. Zaidi ya hayo ni pamoja na maonyesho ya akiolojia, historia ya kiasili, geologi na makusanyo ya kijeshi. Makafadhi haya yamekuwa wazi tangu 1882.
 
 
== Historia ==
Makavazi ya [[Derby]] inaunganisha historia ya kuanzishwa kwake na Mji wa Derby na Jamii ya Makumbusho na historia ya Kiasili mnamo Februari 10, Februari 1836.
Jamii hiyo ilikuwa ya kibinafsi na iligharamiwa na pesa za wanachama. Sanaa zilizohifadhiwa zilikuwa mchango wa kihiari kutoka kwa Dr Forrester aliyekuwa Rais wa Jamii ya philosophia ya Derby. Msimamizi wa makafadi hayo alikuwa ni William Cavendish, 6th Duke of Devonshire na Rais alikuwa ni Sir George Harpur Crewe, 8th Baronet, ambaye alikuwa na nia kubwa ya kuhifadhi vitu vya kisanaa. Kanali George Gawler alichangia katika ukusanyaji wa madini na ndege zilizohifadhiwa ambayo ilikuwa ni pamoja na albatross alizokusanya kutoka kwa muda wake kama gavana katika Australia Kusini. Katika mwaka 1839 kulikuwa na maonyesho makubwa katika taasisi ya mekaniki ambayo ilikuwa na vitu vingi ikiwa ni pamoja na sanaa zilizosanywa na Joseph Strutt. Mengi ya sanaa hizi zilipata kuhifadhiwa katika makafadi ya Derby. Mnamo 1840, Jamii ilihamia eneo la Atheneum katika Victoria Street. Sanaa zilizosanya ziliongezeka kwa wingi mwaka wa 1856.
Mwaka 1857, Llewellyn Jewitt akawa katibu na makafadhi yakafunguliwa wazi kwa umma kwa ujumla kila Jumamosi asubuhi. Mwaka 1858 jamii ya philosophia ya Derby walihamia nyumba ya Wardwick katika Derby kama zimeunganishwa na ikaitwa Makafadhi ya Mji wa Derby County na jamii ya Kihistoria. Hatua hii imejumuisha vitabu vya maktaba ya jamii kiasi cha 4000, hisabati na sayansi na vifaa. Katika mwaka 1863 Mwana sayansi wa mimea Bwana Croall Alexander aliteuliwa Mkutubi wa kwanza na mtunzi wa makafadhi na mwaka uliofuata makafadhi na maktaba yakaunganishwa pamoja. Croall alitoka mwaka wa 1875 na kwenda kuwa mtunza wa Taasisi ya Smith katika Stirling.
Makavazi ya Derby hatimaye ilihamishwiwa usimamizi wa Derby Corporation mnamo 1870, lakini walipata changamoto kwa miaka mitatu ikiwemo ukosefu wa nafasi ya kuwekeza sanaa. Hatimaye Makavazi yalifunguliwa wazi kwa umma mnamo Juni 28, Juni 1879. Nyumba ya sanaa ilifunguliwa 1882 na mwaka wa 1883 yaliunganishiwa stima.
Mnamo mwaka wa 1936, makavazi yalipewa mkusanyiko mkubwa wa picha za kuchora na Alfred E. Goodey ambaye alikuwa amezikusanya kwa muda wa miaka 50. Katika kifo chake mwaka 1945 aliacha £ 13,000 kujenga uga wa makavazi, ambayo ilikamilika mwaka 1964 ukarabati wa sehemu ya majengo mpya na wa zamani ulifanywa katika 2010-2011.