Wanilamba : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
No edit summary
No edit summary
Mstari 9:
 
Walipoanza kuitwa Wanyiramba na Wanyisanzu/Waihanzu
Wakaishi hapo Kisiriri kwa muda mrefu kabla ya kutokea ukame mkubwa sana uliosababisha njaa katika eneo hilo. Ili kukabiliana na tatizo hilo la njaa, watu hao walitumia mboa za majani za mlenda uliokaushwa zijulikanazo kama "ndalu" kama chakula kikuu. Kutokana na kula "ndalu" kwa mtindo wa kulamba, watu wa makabila mengine ya kibantu walivyowaona wakawaita "wenye kulamba" na baadaye likabadilika hadi kuwa "wenyilamba" hadi "Wanyiramba".
Ikumbukwe kuwa hadi hapo Wanyisanzu na Wanyiramba walikuwa kabila moja na wote walifahamika kama Wanyiramba baada ya njaa hiyo.
 
Wanyisanzu/Waihanzu wahamia pori la Mkalama
Kundi moja likaamua kuondoka hapo Kisiriri hadi pori la Mkalama wakiwa na mifugo yao na familia zao na walipofika katika pori hilo ili kujilinda na wanyama wakali wakajenga nyumba na kuzungushia maboma ya miba maarufu kama "masanzu/mahanzu". Baadaye baadhi ya Wanyiramba waliobaki Kisiriri nao waliamua kuondoka hapo na walipofika Mkalama wakawakuta wenzao wamezungushia nyumba zao kwa Maboma ya "masanzu/mahanzu" ndipo walipoanza kuwaita hawa ni wanyisanzu au waihanzu.
 
Wanyiramba na Wanyisanzu japo wanahistoria inayofanana na kwa mtu mgeni anaweza kudhani kuwa hakuna tofauti baina yao, lakini ukweli ni kuwa kuna tofauti kubwa sana baina yao.
 
Koo zao na Wanapopatikana
Wanyiramba
Hizi ni koo tano za Wanyiramba na wanapopatikana
 
•Kinampanda: Wanaishi sehemu za milimani hasa huko Kinampanda